Hamia kwenye habari

Ukumbusho wa Kifo cha Yesu

Jumamosi, Aprili 12, 2025

Mashahidi wa Yehova huadhimisha Ukumbusho wa kifo cha Yesu mara moja kila mwaka kama Yesu alivyoamuru aliposema: “Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka.”​—Luka 22:19.

Tunakukaribisha kuhudhuria tukio hili.

Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi

Programu hiyo itakuwa na urefu gani?

Ni programu ya saa moja hivi.

Programu hiyo itafanyika wapi?

Wasiliana na Mashahidi wa Yehova ili kujua inafanyika wapi katika eneo ulilopo.

Je, ninapaswa kulipa kiingilio?

Hapana.

Je, kuna michango itakayokusanywa?

Hapana.

Ninapaswa kuvalia jinsi gani?

Ingawa hatupangi mavazi maalum yanayopaswa kuvaliwa katika Ukumbusho, Mashahidi wa Yehova hujitahidi kufuata ushauri wa Biblia kuhusu kuvalia kwa kiasi na kwa heshima. (1 Timotheo 2:9) Huhitaji kuvalia mavazi ya gharama au mavazi ya sherehe.

Ni nini kitakachofanywa kwenye Ukumbusho huo?

Mkutano huo huanza na kumalizika kwa wimbo, na pia sala inatolewa na mhudumu wa Mashahidi wa Yehova. Kutakuwa na hotuba inayozungumzia umuhimu wa kifo cha Yesu na jinsi tunavyonufaika kutokana na kile ambacho Mungu na Kristo wametufanyia.

Ukumbusho wa mwaka wa 2025 na 2026 utafanywa tarehe gani?

2025: Jumamosi, Aprili 12

2026: Alhamisi, Aprili 2