Hamia kwenye habari

Je, Mungu Alimuumba Ibilisi Ili Atujaribu?

Je, Mungu Alimuumba Ibilisi Ili Atujaribu?

Jibu la Biblia

 Biblia inaonyesha kwamba Mungu hakumuumba Ibilisi. Badala yake, Mungu aliumba kiumbe aliyegeuka na kuwa Ibilisi. Kuhusiana na Mungu, Biblia inasema: “Kazi zake ni kamilifu, kwa maana njia zake zote ni haki. Mungu wa uaminifu, ambaye hana ukosefu wowote wa haki; Yeye ni mwadilifu na mnyoofu.” (Kumbukumbu la Torati 32:3-5) Kupatana na andiko hilo, tunaweza kusema kuwa mwanzoni Shetani Ibilisi alikuwa mkamilifu na mwadilifu, yaani, alikuwa mmoja wa malaika wa Mungu.

 Katika Yohana 8:44, Yesu alisema kuwa Ibilisi “hakusimama imara katika kweli,” akimaanisha kuwa kuna wakati ambapo Shetani hakuwa mwongo wala mwenye hatia.

 Hata hivyo, kama viumbe wengine wenye akili wa Yehova, malaika aliyegeuka kuwa Shetani alikuwa na uhuru wa kuchagua kati ya mema na mabaya. Kwa kuchagua kumpinga Mungu na kuwachochea wanadamu wawili wa kwanza wajiunge naye, alijifanya mwenyewe kuwa Shetani, jina linalomaanisha “Mpinzani.”—Mwanzo 3:1-5; Ufunuo 12:9.