Hamia kwenye habari

Kuna Sababu Gani Mbili Kwa Nini Mungu Hajibu Sala Nyingine?

Kuna Sababu Gani Mbili Kwa Nini Mungu Hajibu Sala Nyingine?

Jibu la Biblia

 Kuna sala ambazo Mungu hajibu. Chunguza mambo mawili yanayoweza kumfanya Mungu asijibu sala.

1. Sala hiyo haipatani na mapenzi ya Mungu

 Mungu hajibu maombi yanayopingana na mapenzi, au matakwa yake yanayopatikana katika Biblia. (1 Yohana 5:14) Kwa mfano, Biblia inatuambia tuepuke pupa. Kucheza kamari huchochea pupa. (1 Wakorintho 6:9, 10) Kwa hiyo, Mungu hatajibu sala yako ya kuomba ushinde tiketi ya bahati-nasibu. Mungu si kama jini unaloliita kukutimizia lolote unalotaka. Kwa kweli unapaswa kushukuru kwamba hayuko hivyo. Angekuwa hivyo, ungehofia mambo ambayo watu wengine wangemwomba Mungu afanye.—Yakobo 4:3.

2. Yule anayesali anamwasi Mungu

 Mungu hasikilizi sala za watu wanaotaka kumchukiza kwa matendo yao. Kwa mfano, Mungu aliwaambia hivi watu waliodai kumtumikia lakini walikuwa wakimwasi: “Hata mjapotoa sala nyingi, mimi sisikilizi; mikono yenu imejaa umwagaji wa damu.” (Isaya 1:15) Lakini ikiwa wangebadili njia zao na ‘kunyoosha mambo’ kati yao na Mungu, angesikiliza sala zao.—Isaya 1:18.