Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

 JE, NI KAZI YA UBUNI?

Uwezo Hafifu wa Kuona wa Buibui Anayeruka

Uwezo Hafifu wa Kuona wa Buibui Anayeruka

BUIBUI anayeruka (jumping spider), ana uwezo wa pekee wa kuona unaomwezesha kupima umbali hususa anaohitaji kuruka. Buibui huyo hufanyaje hivyo?

Fikiria hili: Ili kupima umbali kutoka kwenye kitu fulani, buibui huyo hutumia sehemu ya pekee ya macho yake mawili makubwa, kila jicho lina retina iliyo na matabaka kadhaa ya chembe zinazopokea nuru. Matabaka mawili kati ya hayo hupokea nuru ya rangi ya kijani. Tabaka moja hupokea picha ya rangi hiyo ikiwa wazi kabisa na tabaka lile lingine hupokea picha ya rangi hiyo ikiwa hafifu. Picha ya kitu inapoonekana kuwa si wazi kabisa, machoni pa buibui huyo picha hiyo iko karibu zaidi. Jambo hilo humwezesha buibui kujua ataruka umbali gani hususa ili kukamata windo lake.

Watafiti wangependa kuiga mbinu ya buibui huyo ili kutokeza kamera zenye uwezo wa kuona kwa njia ya wazi zaidi na pia roboti zinazoweza kupima kitu kiko mbali kadiri gani. Kulingana na tovuti ya habari inayoitwa ScienceNOW, uwezo wa kuona wa buibui huyo ni “mfano mzuri wa jinsi wanyama wenye urefu wa milimita tano walio na ubongo mdogo zaidi kuliko ule wa nzi wanavyoweza kukusanya na kutenda kupatana na habari tata sana wanayoona.”

Una maoni gani? Jinsi buibui anayeruka anavyoutumia uwezo wake hafifu wa kuona, ni jambo lililojitokeza lenyewe? Au lilibuniwa?