Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HABARI KUU | UHAI ULIANZAJE?

Jibu Linaloridhisha

Jibu Linaloridhisha

BAADA ya kuchunguza uthibitisho watu wengi wamekubali kwamba viumbe hai viliumbwa. Fikiria mfano wa Antony Flew, profesa wa falsafa ambaye pindi moja alikuwa mtetezi wa fundisho la kwamba hakuna Mungu. Alipojifunza kuhusu sheria za asili za ulimwengu na viumbe mbalimbali, Flew alibadili maoni yake. Akinukuu msemo wa wanafalsafa wa kale aliandika: “Tunapaswa kukubali jibu sahihi hata ikiwa si jibu tulilotarajia.” Profesa Flew alikubali uthibitisho unaoonyesha kwamba kuna Muumba.

Gerard, aliyetajwa katika makala iliyotangulia anaamini kwamba kuna Muumba. Ingawa amesoma sana na ni mwanasayansi, alisema hivi: “Sikupata uthibitisho wowote kwamba uhai ulitokana na vitu visivyo hai. Kwa kuwa kuna mpangilio mzuri ulimwenguni na viumbe wengi wa pekee, basi lazima kuwe na Aliyebuni na Kupanga mambo yote.”

Kama vile mtu anavyoweza kumjua mchoraji kwa kuchunguza michoro yake, Gerard alijua sifa za Muumba kwa kuchunguza uumbaji. Pia alijifunza Biblia, kitabu cha Mungu. (2 Timotheo 3:16) Katika Biblia alipata majibu ya maswali kuhusu chanzo cha uhai na suluhisho la matatizo ya wanadamu. Basi akaamini kwamba Biblia pia ilitungwa na Mungu.

Kama Gerard alivyosema, Biblia ina majibu mazuri yanayoridhisha. Tunakuhimiza uyachunguze.