Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HABARI KUU | JE, BIBLIA INA FAIDA LEO?

Viwango Vinavyomfaa Kila Mtu, Nyakati Zote—Kujizuia

Viwango Vinavyomfaa Kila Mtu, Nyakati Zote—Kujizuia

KANUNI YA BIBLIA: “Mtu mjinga huiachilia roho yake yote, lakini mwenye hekima huituliza mpaka mwisho.”Methali 29:11.

“Nahisi kwamba nilinusurika kifo!”

FAIDA: Ikiwa ungeorodhesha faida zinazotokana na kuwa na sifa ya kujizuia, bila shaka ungehitaji rundo la karatasi! Kwa ufupi, sifa hii hutulinda kiafya. Biblia husema hivi: “Moyo mtulivu ni uzima wa mwili wenye nyama.” Pia inasema, “Moyo wenye shangwe ni dawa nzuri.” (Methali 14:30; 17:22) Utafiti umeonyesha kwamba watu wakali na wanaopenda kukasirika ovyoovyo wanaweza kupata matatizo ya afya na hasa ugonjwa wa moyo. Kwa kweli, kuwa na sifa ya kujizuia kuna faida nyingi.

Cassius, ambaye ana umri wa miaka 30 hivi anasema: “Nilipenda mabishano na nilikasirika upesi, na mara kwa mara pia nilipenda kupigana. Sikujiheshimu. Lakini nilipoanza kufuata kanuni za Biblia mambo yalibadilika. Nilijifunza jinsi ya kudhibiti hasira, kuwa mnyenyekevu, na hata kuwasamehe wengine. Nisingefanya hivyo, leo hii ningekuwa gerezani. Kusema kweli, nahisi kwamba nilinusurika kifo!”

Cassius alijifunza kudhibiti hasira na kuwasamehe wengine