Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 117

Sifa ya Wema

Sifa ya Wema

(2 Mambo ya Nyakati 6:41)

  1. 1. Yehova Mungu wa Wema,

    Twaona wema wako.

    Wewe ni mtakatifu,

    Njia zako ni njema.

    Watuonyesha fadhili

    Tusizozistahili.

    Unastahili ibada,

    Ndiwe twatumikia.

  2. 2. Watu wako waonyesha,

    Sifa ya wema wako,

    Katika mwenendo wao,

    Na wanapohubiri.

    Mafundisho yako mema,

    Yawachochea wengi.

    Twakuomba roho yako,

    Tuwe wema daima.

  3. 3. Ubariki wema wetu,

    Kwa ndugu zetu wote.

    Tuonyeshe watu wote,

    Fadhili zako Mungu.

    Familia, Kutaniko,

    Mijini, vijijini.

    Bariki juhudi zetu,

    Tuwe wema milele.