WIMBO NA. 3
Tumaini, Nguvu, na Uhakika Wetu
-
1. Yehova umetupatia
tumaini bora.
Latusisimua sana,
tutalitangaza.
Mahangaiko ya maisha,
hutufanya tuhofu.
Nalo tumaini letu
Linadhoofika.
(KORASI)
Tumaini, nguvu,
na uhakika;
zatoka kwako Yehova.
Ili tuhubiri
kwa uhakika,
twakutegemea wewe.
-
2. Ichochee mioyo yetu,
tusikusahau.
Watufariji daima,
tunapolemewa.
Kutafakari wema wako,
kunatuimarisha.
Tuwajulishe wengine
jina lako kuu.
(KORASI)
Tumaini, nguvu,
na uhakika;
zatoka kwako Yehova.
Ili tuhubiri
kwa uhakika,
twakutegemea wewe.
(Ona pia Zab. 72:13, 14; Met. 3:5, 6, 26; Yer. 17:7.)