Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 3

Tumaini, Nguvu, na Uhakika Wetu

Tumaini, Nguvu, na Uhakika Wetu

(Methali 14:26)

  1. 1. Yehova umetupatia

    tumaini bora.

    Latusisimua sana,

    tutalitangaza.

    Mahangaiko ya maisha,

    hutufanya tuhofu.

    Nalo tumaini letu

    Linadhoofika.

    (KORASI)

    Tumaini, nguvu,

    na uhakika;

    zatoka kwako Yehova.

    Ili tuhubiri

    kwa uhakika,

    twakutegemea wewe.

  2. 2. Ichochee mioyo yetu,

    tusikusahau.

    Watufariji daima,

    tunapolemewa.

    Kutafakari wema wako,

    kunatuimarisha.

    Tuwajulishe wengine

    jina lako kuu.

    (KORASI)

    Tumaini, nguvu,

    na uhakika;

    zatoka kwako Yehova.

    Ili tuhubiri

    kwa uhakika,

    twakutegemea wewe.