Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 90

Tianeni Moyo

Tianeni Moyo

(Waebrania 10:24, 25)

  1. 1. Tuwatiapo ndugu moyo,

    Kumtumikia Mungu,

    Upendo unaimarika;

    Kwawa amani, umoja.

    Upendo wa watu wa Mungu,

    Hufanya tuvumilie.

    Kutaniko ni kimbilio,

    Mahali pa usalama.

  2. 2. Neno zuri linaposemwa,

    Lafurahisha moyo, we!

    Maneno yenye kufariji

    Ya ndugu zetu wapendwa.

    Tufanyapo kazi pamoja,

    Na ndugu na dada zetu,

    Tunaimarishana nao,

    Mizigo twabebeana.

  3. 3. Siku ya Yehova karibu.

    Twaiona kwa imani.

    Tunahitaji mikutano,

    Tubaki katika njia.

    Milele tutatumikia,

    Na watu wake Yehova.

    Daima tutiane moyo,

    Tuwe washikamanifu.