Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 96

Kitabu cha Mungu Ni Hazina

Kitabu cha Mungu Ni Hazina

(Methali 2:1)

  1. 1. Kuna kitabu ambacho huwapa,

    Watu amani na tumaini.

    Mawazo yake yana nguvu nyingi;

    Kinafumbua macho ya watu.

    Ni Biblia takatifu ya Mungu.

    Iliandikwa kale na watu.

    Waliompenda sana Yehova,

    Walichochewa na roho yake.

  2. 2. Waliandika kuhusu ’umbaji,

    Ulimwengu ulivyotokea.

    Ukamilifu wa mtu mwanzoni.

    Paradiso ilivyopotea.

    Pia kuhusu malaika mwovu,

    Aliyeipinga enzi kuu.

    Kukawa dhambi, kifo, na huzuni,

    Ushindi wa Yah waja upesi.

  3. 3. Leo twaishi pindi ya pekee.

    Ufalme wa Mungu watawala.

    Twatangaza habari za Ufalme,

    Na baraka zitakazokuja.

    Biblia inazo habari njema;

    Ni karamu tele ya kiroho.

    Huwapa watu wote tumaini;

    Hiyo ni hazina kwelikweli.