Hamia kwenye habari

Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Hawapaiti Mahali Pao pa Ibada Kanisa?

Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Hawapaiti Mahali Pao pa Ibada Kanisa?

 Katika Biblia, neno la Kigiriki ambalo mara nyingine hutafsiriwa “kanisa” humaanisha kikundi cha waabudu, si jengo wanamokutania.

 Ona mfano ufuatao: Mtume Paulo alipowaandikia barua Wakristo huko Roma, alituma salamu kwa wenzi wa ndoa Akila na Priska, kisha akaongezea hivi: “Nisalimieni na kanisa lililomo katika nyumba yao.” (Waroma 16:4, Union Version) Paulo hakukusudia kutuma salamu zake kwa jengo. Badala yake, alikuwa akituma salamu kwa watu waliokutana katika nyumba hiyo. *

 Kwa sababu hiyo, badala ya kuita mahali petu pa ibada kanisa, sisi hupaita “Jumba la Ufalme.”

Kwa nini panaitwa “Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova”?

 Jina hilo linafaa kwa sababu zifuatazo:

  •   Jengo hilo ni jumba, au mahali pa kukutania.

  •   Sisi hukutanika hapo ili kumwabudu Yehova, Mungu anayetajwa katika Biblia, na ili kutoa ushahidi kumhusu.​—Zaburi 83:18; Isaya 43:12.

  •   Sisi pia hukutanika hapo ili kujifunza kuhusu Ufalme wa Mungu, ambao Yesu alizungumza sana kuuhusu.​—Mathayo 6:9, 10; 24:14; Luka 4:43.

 Unaalikwa utembelee Jumba la Ufalme lililo karibu na eneo unaloishi ujionee mwenyewe jinsi Mashahidi wa Yehova wanavyofanya mikutano yao.

^ Maneno yanayofanana na hayo yanapatikana kwenye 1 Wakorintho 16:19; Wakolosai 4:15; na Filemoni 2.