Hamia kwenye habari

Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulimwenguni Pote—Tukio la Kihistoria

Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulimwenguni Pote—Tukio la Kihistoria

Ujenzi wa makao makuu ya ulimwenguni pote ya Mashahidi wa Yehova unaendelea huko Warwick, New York. Asilimia kubwa ya watu wanaoshiriki katika ujenzi huo ni wajitoleaji ambao wametoka sehemu mbalimbali nchini Marekani, nao wanafuata ratiba ya ujenzi yenye shughuli nyingi kwelikweli. Wanafanya hivyo kwa hiari, kwa bidii, bila kutarajia malipo yoyote, nao wanaona kufanya hivyo kuwa ni zawadi kwa Mungu. Tazama video hii ujionee jinsi kikundi hicho cha wajitoleaji kinavyofanya kazi hiyo kubwa!