Ona video zinazopatikana

Armagedoni Ni Nini?

Armagedoni Ni Nini?

Jibu ya Biblia

 Armagedoni ni vita ya mwisho kati ya Mungu na serikali za wanadamu. Hata sasa zile serikali na wale wenye kuziunga mukono zinamupinga Mungu na zinakatala kumutii. (Zaburi 2:2) Vita ya Armagedoni itaharibu serikali za wanadamu.​—Danieli 2:44.

 Neno “Armagedoni” inapatikana mara moya tu mu Biblia, mu Ufunuo 16:16. Unabii wenye kuwa mu ile andiko unaonyesha kama “wafalme wa dunia yote yenye kuikaliwa na watu” watakusanywa “pamoja mahali kwenye kunaitwa katika Kiebrania Armagedoni” “kwa ajili ya vita ya ile siku kubwa ya Mungu Mweza-Yote.”​—Ufunuo 16:14.

 Nani njo watapigana vita ya Armagedoni? Yesu ataongoza majeshi ya mbinguni yenye itapigana na maadui wa Mungu na kuwashinda. (Ufunuo 19:11-​16, 19-​21) Maadui wa Mungu ni wale wote wenye kupinga mamlaka yake na wenye hawamuheshimie.​—Ezekieli 39:7.

 Vita ya Armagedoni itafanyika mu eneo ya Mashariki ya Kati? Hapana. Haitapiganwa mu eneo moya tu, lakini mu dunia yote.​—Yeremia 25:32-​34; Ezekieli 39:17-​20.

 Neno Armagedoni, yenye wakati fulani inaandikwa “Har–​Magedoni” (mu Kiebrania Har Meghiddohnʹ), maana yake “Mulima wa Megido.” Megido ilikuwa muji mu Israeli ya zamani. Historia inaonyesha kama vita kubwa-kubwa zilifanyika karibu na Megido. Na Biblia inazungumuzia vita fulani kati ya zile vita. (Waamuzi 5:19, 20; 2 Wafalme 9:27; 23:29) Lakini, Armagedoni haiwezi kuwa eneo fulani karibu na Megido ya zamani. Hakuna mulima mukubwa wenye unapatikana kule, na wale wenye kupigana na Mungu hawawezi kuenea hata mu Eneo Tambarare ya Yezreeli yenye inapatikana karibu na Megido. Armagedoni ni wakati serikali zote za wanadamu zitajiunga pamoya juu ya kupigana na serikali ya Mungu.

 Vita ya Armagedoni itakuwa namna gani? Hatujue vile Mungu atatumia nguvu yake. Lakini anaweza kutumia silaha zenye alitumiaka zamani, sawa vile mvua ya majiwe, matetemeko ya inchi, mvua kubwa, moto na kiberiti, radi, na magonjwa. (Yobu 38:22, 23; Ezekieli 38:19, 22; Habakuki 3:10, 11; Zekaria 14:12) Maadui fulani wa Mungu watavurugika, na kuanza kuuana. Lakini ku mwisho, watafikia kuelewa kama Mungu njo iko napigana nao.​—Ezekieli 38:21, 23; Zekaria 14:13.

 Armagedoni njo itakuwa mwisho wa dunia? Dunia haitaharibiwa ku Armagedoni juu Mungu ameipatia wanadamu juu waishi juu yake milele. (Zaburi 37:29; 96:10; Muhubiri 1:4) Haiko wanadamu wote njo wataharibiwa ku Armagedoni, juu “kundi kubwa” ya watu wenye kumutumikia Mungu wataokoka.​—Ufunuo 7:9, 14; Zaburi 37:34.

 Mu Biblia, neno “dunia” inamaanisha hii planete yenye tunaishi ndani. Lakini wakati fulani inamaanisha pia watu wabaya wenye kumupinga Mungu. (1 Yohana 2:15-​17) Kwa hiyo, wakati Biblia inasema kama Armagedoni italeta “mwisho wa dunia,” inamaanisha kama italeta mwisho wa watu wabaya.​—Matayo 24:3, La Sainte Bible en swahili de la R.D Congo.

 Vita ya Armagedoni itatokea wakati gani? Wakati Yesu alikuwa nazungumuzia “taabu kubwa,” yenye sehemu yake ya mwisho ni Armagedoni, alisema hivi: “Kuhusu siku ile na saa ile, hakuna mutu mwenye anajua, ikuwe malaika wa mbinguni ao Mwana, lakini Baba tu.” (Matayo 24:21, 36) Lakini, Biblia inaonyesha kama Armagedoni itatokea wakati wa kuwapo kwa Yesu kwenye hakuonekane, kwenye kulianza mu mwaka wa 1914.​—Matayo 24:37-​39.