Je, Shetani Anaweza Kuwatawala Wanadamu?
Jibu la Biblia
Shetani na mashetani wanaongoza watu wafanye mabaya sana. Kwa hiyo Biblia inasema: ‘Yule Muovu anautawala ulimwengu wote.’ (1 Yohana 5:19, New Century Version) Biblia inaonyesha njia ambazo Shetani anatumia ili kuwatawala watu.
Ujanja. Biblia inatia Wakristo moyo ‘wapambane na ujanja wa Shetani.’ (Waefeso 6:11, NCV) Njia moja ya ujanja ambayo anatumia ni kuwafanya watu waamini kwamba watu wake ni watumishi wa Mungu.—2 Wakorintho 11:13-15.
Kupashana habari na mashetani. Shetani anadanganya watu kupitia wachawi, watu wa kutabiri mambo, na wote wanaotumia uaguzi ao wale wanaochunguza nyota. (Kumbukumbu 18:10-12) Matumizi ya dawa za kulewesha, kulalisha usingizi, njia zingine za kupoteza akili zinafanya pia mutu aongozwe na mashetani.—Luka 11:24-26.
Dini ya uongo. Dini zinazofundisha mambo ya uongo zinawafanya watu wasimutii Mungu. (1 Wakorintho 10:20) Biblia inaita mambo hayo ya uongo kuwa “mafundisho ya roho waovu.”—1 Timotheo 4:1.
Kuingia katika watu. Biblia inasimulia habari za roho waovu wanaoingia katika watu na kuwaongoza. Wakati mwengine mashetani yanafanya watu kuwa vipofu ao mabubu na hata kuwafanya wajiumize.—Mathayo 12:22; Marko 5:2-5.
Namna ya kuepuka kuongozwa na Shetani
Usiogope mashetani, kwa kuwa Biblia inaonyesha namna unavyoweza kumupinga kabisa Shetani:
Jifunze njia za Shetani ili ‘usikose kujua mbinu zake.’—2 Wakorintho 2:11.
Jifunze Biblia na kisha utumie mambo unayojifunza. Tumia kanuni za Biblia ili zikuepushe na uvutano mubaya wa Shetani.—Waefeso 6:11-18.
Achana kabisa na kila kitu kinachoweza kukuunganisha na mashetani. (Matendo 19:19) Hiyo inatia ndani, muziki, vitabu, magazeti, picha, na video zinazohusu kupashana habari na mashetani.