Ona video zinazopatikana

Je, Shetani Anaweza Kuwatawala Wanadamu?

Je, Shetani Anaweza Kuwatawala Wanadamu?

Jibu la Biblia

 Shetani na mashetani wanaongoza watu wafanye mabaya sana. Kwa hiyo Biblia inasema: ‘Yule Muovu anautawala ulimwengu wote.’ (1 Yohana 5:​19, New Century Version) Biblia inaonyesha njia ambazo Shetani anatumia ili kuwatawala watu.

  •   Ujanja. Biblia inatia Wakristo moyo ‘wapambane na ujanja wa Shetani.’ (Waefeso 6:​11, NCV) Njia moja ya ujanja ambayo anatumia ni kuwafanya watu waamini kwamba watu wake ni watumishi wa Mungu.​—2 Wakorintho 11:13-​15.

  •   Kupashana habari na mashetani. Shetani anadanganya watu kupitia wachawi, watu wa kutabiri mambo, na wote wanaotumia uaguzi ao wale wanaochunguza nyota. (Kumbukumbu 18:10-​12) Matumizi ya dawa za kulewesha, kulalisha usingizi, njia zingine za kupoteza akili zinafanya pia mutu aongozwe na mashetani.​—Luka 11:24-​26.

  •   Dini ya uongo. Dini zinazofundisha mambo ya uongo zinawafanya watu wasimutii Mungu. (1 Wakorintho 10:20) Biblia inaita mambo hayo ya uongo kuwa “mafundisho ya roho waovu.”​—1 Timotheo 4:1.

  •   Kuingia katika watu. Biblia inasimulia habari za roho waovu wanaoingia katika watu na kuwaongoza. Wakati mwengine mashetani yanafanya watu kuwa vipofu ao mabubu na hata kuwafanya wajiumize.​—Mathayo 12:22; Marko 5:​2-5.

Namna ya kuepuka kuongozwa na Shetani

 Usiogope mashetani, kwa kuwa Biblia inaonyesha namna unavyoweza kumupinga kabisa Shetani:

  •   Jifunze njia za Shetani ili ‘usikose kujua mbinu zake.’​—2 Wakorintho 2:​11.

  •   Jifunze Biblia na kisha utumie mambo unayojifunza. Tumia kanuni za Biblia ili zikuepushe na uvutano mubaya wa Shetani.​—Waefeso 6:​11-​18.

  •   Achana kabisa na kila kitu kinachoweza kukuunganisha na mashetani. (Matendo 19:19) Hiyo inatia ndani, muziki, vitabu, magazeti, picha, na video zinazohusu kupashana habari na mashetani.