Ona video zinazopatikana

Sababu Gani Mungu Hasikilize Sala Fulani za Watu?

Sababu Gani Mungu Hasikilize Sala Fulani za Watu?

Jibu la Biblia

 Kuna sala ambazo Mungu hasikilize. Fikiria sababu mbili zinazoweza kumufanya Mungu akatae kusikiliza sala.

1. Ikiwa sala haipatane na mapenzi ya Mungu

 Mungu hasikilize sala zinazopingana na mapenzi yake, ao kanuni zake. (1 Yohana 5:14) Kwa mufano, Biblia inatuomba tuepuke tamaa isiyofaa. Muchezo wa feza unamufanya mutu awe na tamaa ya feza. (1 Wakorintho 6:​9, 10) Kwa hiyo, Mungu hatajibu sala yako ikiwa unamuomba akusaidie ushinde katika muchezo wa feza ao tombola. Mungu si roho inayoweza kutuletea bahati. Bila shaka, tunapaswa kufurahi kwa kuwa yeye haiko hivyo. Ikiwa angekuwa hivyo, basi ungepaswa kuogopa wale wengine wanaocheza, kwa sababu wao pia wanaomba Mungu bahati.—Yakobo 4:3.

2. Ikiwa mutu anayesali anatenda mambo mabaya

 Mungu hasikilize sala za wale wanaokusudia kufanya tu matendo yanayomuchukiza. Kwa mufano, Mungu aliwaambia hivi wale waliodai kwamba wanamutumikia lakini ambao walitenda mambo mabaya: ‘Nanyi munaponyoosha mikono yenu, mimi naficha macho yangu kutoka kwenu. Hata mujapotoa sala nyingi, mimi sisikilize; mikono yenu imejaa umwangaji wa damu.’ (Isaya 1:15) Ikiwa wangebadili njia zao na ‘kunyoosha mambo’ pamoja na Mungu, angesikiliza sala zao.—Isaya 1:18.