Ya Pili kwa Wakorinto 9:1-15

  • Kitia-moyo cha kutoa (1-15)

    • Mungu anapenda mutu mwenye anatoa kwa furaha (7)

9  Sasa kuhusu utumishi kwa ajili ya watakatifu,+ haiko lazima kabisa niwaandikie ninyi,  kwa maana ninajua utayari wenu wenye ninajisifia kwa Wamakedonia, kwamba Akaya imekwisha kuwa tayari tangu mwaka mumoja sasa, na bidii yenu imechochea wengi kati yao.  Lakini ninatuma ndugu, ili kujisifu kwetu juu yenu kusionekane kuwa bure kuhusu jambo hilo, na kwamba mukuwe tayari kwelikweli, kama vile nilisema mutakuwa.  Tofauti na hilo, kama Wamakedonia wanakuja pamoja na mimi na kukuta hamuko tayari, sisi​—na hata ninyi​—tutasikia haya kwa sababu tunawatumainia ninyi.  Basi niliona kama ni jambo la lazima kutia ndugu moyo wakuje kwenu mbele ya wakati na watayarishe zawadi yenu yenye munatoa kwa utayari, zawadi yenye iliahidiwa, ili ikuwe tayari kama zawadi ya ukarimu, hapana kama kitu chenye kunyanganywa.  Lakini juu ya jambo hili, mutu yeyote mwenye anapanda kwa uchoyo atavuna pia kwa uchoyo, na mutu yeyote mwenye anapanda kwa wingi atavuna pia kwa wingi.+  Kila mumoja afanye kama vile alikusudia katika moyo wake, haiko kwa kutokupenda* wala kwa kulazimishwa,+ kwa maana Mungu anapenda mutu mwenye anatoa kwa furaha.+  Zaidi ya hayo, Mungu anaweza kufanya fazili zake zote zenye hazistahiliwe zikuwe nyingi kuwaelekea ninyi, ili sikuzote mukuwe wenye kutosheka kabisa katika kila jambo, na pia mukuwe na vitu vingi kwa ajili ya kila kazi njema.+  (Kama vile imeandikwa: “Amegawa kwa wingi;* amepatia maskini. Haki yake inadumu milele.”+ 10  Sasa Ule mwenye anapatia mupandaji mbegu kwa wingi na mukate wa kula, atawapatia ninyi na kuwaongezea mbegu ili mupande, na ataongeza mavuno ya haki.) 11  Katika kila jambo munatajirishwa kwa ajili ya kila namna ya ukarimu, wenye kupitia sisi unatokeza shukrani kwa Mungu; 12  kwa sababu utumishi wa kazi hii ya watu wote haiko tu kutimiza muzuri mambo yenye watakatifu wako nayo+ lazima lakini pia ni ili kuwa tajiri katika shukrani nyingi kwa Mungu. 13  Kupitia uhakikisho wenye unatolewa na utumishi huu wa kutoa musaada, wanamutukuza Mungu kwa sababu munajitiisha kwa habari njema juu ya Kristo, kama vile mulitangaza mbele ya watu wote, na kwa sababu ninyi muko wakarimu katika muchango wenu kwa ajili yao na kwa ajili ya wote.+ 14  Na kwa kumulilia Mungu* kwa ajili yenu, wanaonyesha kwamba wanawapenda ninyi kwa sababu ya fazili nyingi sana zenye hazistahiliwe za Mungu juu yenu. 15  Mungu apewe shukrani kwa ajili ya zawadi yake ya bure yenye haiwezi kuelezeka.

Maelezo ya Chini

Ao “kutokutaka.”
Ao “kwa ukarimu.”
Ao “kuomba dua.”