Ufunuo kwa Yohana 12:1-17

  • Mwanamuke, mutoto mwanaume, na nyoka mukubwa (1-6)

  • Mikaeli anapigana na ule nyoka mukubwa (7-12)

    • Nyoka mukubwa anatupwa katika dunia (9)

    • Ibilisi anajua kwamba iko na kipindi kifupi (12)

  • Nyoka mukubwa anamutesa mwanamuke (13-17)

12  Kisha alama kubwa ikaonekana mbinguni: Mwanamuke mumoja+ alikuwa amepambwa* jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake kulikuwa taji la nyota kumi na mbili (12),  na alikuwa na mimba. Na alikuwa analia katika maumivu yake na katika uchungu wake wa kuzaa.  Alama ingine ikaonekana mbinguni. Angalia! Nyoka mukubwa wa rangi ya moto,+ mwenye vichwa saba (7) na pembe kumi (10) na mataji* saba juu ya vichwa vyake;  na mukia wake unakokota sehemu moja ya tatu (1/3) ya nyota za mbinguni, na akazitupa chini katika dunia.+ Na ule nyoka mukubwa akaendelea kusimama mbele ya ule mwanamuke+ mwenye alikuwa karibu kuzaa, ili wakati atazaa, ameze mutoto wake.  Na ule mwanamuke akamuzaa mwana,+ mwanaume, mwenye atachunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma.+ Na mutoto wake akanyakuliwa* mupaka kwa Mungu na kwenye kiti chake cha ufalme.  Na ule mwanamuke akakimbilia katika jangwa, kwenye iko* na mahali kwenye kulitayarishwa na Mungu na kwenye watamukulisha kwa siku elfu moja mia mbili makumi sita (1260).+  Na mara moja vita ikatokea mbinguni: Mikaeli*+ na malaika wake wakapigana na ule nyoka mukubwa, na ule nyoka mukubwa na malaika wake wakapigana  lakini hawakushinda,* na mahali hapakupatikana tena mbinguni kwa ajili yao.  Basi ule nyoka mukubwa+ akatupwa chini, ule nyoka wa zamani,+ mwenye kuitwa Ibilisi+ na Shetani,+ mwenye anapotosha dunia yote yenye kuikaliwa na watu;+ akatupwa chini katika dunia,+ na malaika wake wakatupwa chini pamoja naye. 10  Nikasikia sauti kubwa mbinguni ikisema: “Sasa kumekuwa wokovu+ na nguvu na Ufalme wa Mungu wetu+ na mamlaka ya Kristo wake, kwa sababu mushitaki wa ndugu zetu ametupwa chini, mwenye anawashitaki muchana na usiku mbele ya Mungu wetu!+ 11  Na wakamushinda+ kwa sababu ya damu ya Mwana-Kondoo+ na kwa sababu ya neno lao la kutoa ushahidi,+ na hawakupenda nafsi zao*+ hata wakati walipambana na kifo. 12  Kwa sababu hiyo mufurahi, ninyi mbingu na ninyi wenye kukaa ndani yake! Ole wa dunia na wa bahari,+ kwa sababu Ibilisi ameshuka kwenu, akiwa na kasirani kali, akijua kwamba iko* na kipindi kifupi cha wakati.”+ 13  Sasa wakati ule nyoka mukubwa aliona kwamba ametupwa chini katika dunia,+ alimutesa ule mwanamuke+ mwenye alizaa mutoto mwanaume. 14  Lakini ule mwanamuke akapewa mabawa mbili ya tai mukubwa,+ ili aruke kuenda katika jangwa mahali pake, kwenye atakulishwa kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati*+ mbali na uso wa ule nyoka.+ 15  Na ule nyoka akatapika maji kama muto kutoka katika kinywa chake nyuma ya ule mwanamuke, ili kumuzamisha katika muto huo. 16  Lakini dunia ikakuja kumusaidia ule mwanamuke, na dunia ikafungua kinywa chake na kumeza ule muto wenye ule nyoka mukubwa alitapika kutoka katika kinywa chake. 17  Basi ule nyoka mukubwa akakuwa na kasirani kali kumuelekea ule mwanamuke, na akaenda kupigana vita na wale wenye kubakia wa uzao wa* ule mwanamuke,+ wenye wanashika amri za Mungu na wenye wako na kazi ya kutoa ushahidi juu ya Yesu.+

Maelezo ya Chini

Ao “amevaa.”
Ao “mataji ya kifalme.”
Ao “akachukuliwa.”
Ao “eko.”
Maana yake “Ni Nani Mwenye Kuwa Kama Mungu?”
Ao pengine, “lakini alishindwa [ni kusema, ule nyoka mukubwa].”
Ao “uzima wao.” Angalia Maana ya Maneno.
Ao “eko.”
Ni kusema, nyakati tatu na nusu.
Tnn., “mbegu ya.”