Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mafundisho Yenye Inatupatia Tumaini

Mafundisho Yenye Inatupatia Tumaini

Mungu alishalaga kama mu masiku ya mbele kutakuwa mabadiliko ya ajabu. Atamaliza mateso na kupatia wanadamu maisha ya furaha hapa ku dunia. (Zaburi 37:11) Juu ya nini tuamini ile mambo? Ni juu “Mungu haiko mwanadamu bure mwenye anasemaka uongo.” (Hesabu 23:19) Tuone mambo ya muzuri yenye Muumbaji wetu atafanya.

Mungu Atatosha Watu Wabaya

“Wakati waovu wanachipuka kama magugu na wakati wakosaji wote wanasitawi, ni ili waharibiwe milele.”​—ZABURI 92:7.

Vile tuliona mu habari yenye ilipita, mambo ya mubaya iko naendelea kuongezeka. Ile haipaswe kutushangaza. Mu 2 Timoteo 3:1-5, Biblia ilikuwa ilishaonyesha kama mu “siku za mwisho” watu wangekuwa wabaya sana. Siku za mwisho za nini? Siku za mwisho za watu wenye hawamuogope Mungu. Mungu iko karibu kuharibu watu wote wenye wanakatala kubadilisha mwenendo yao ya mubaya. Ni watu wazuri tu, ni kusema wale wenye wanamutii Mungu, njo watabakia ku dunia. “Wenye haki watariti dunia, na wataishi milele juu yake.”​—Zaburi 37:29.

Mungu Atamuharibu Shetani

“Mungu mwenye anatoa amani atamuponda Shetani.”​—WAROMA 16:20.

Wakati Shetani na pepo wachafu hawatakuwa tena, na wakati mambo yote ya mubaya haitakuwa tena, amani itayala mu dunia yote. Muumbaji wetu anasema hivi: ‘Hakuna mutu mwenye atakuogopesha.’​—Mika 4:4.

Mungu Atamaliza Magonjwa na Kifo

“Hema ya Mungu iko pamoja na wanadamu . . . Na atapanguza kila chozi katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena.”​—UFUNUO 21:3, 4.

Mateso na magonjwa itaisha sababu Mungu atatosha mambo yote ya mubaya yenye iko natupata juu ya Shetani, Adamu, Eva, na juu ya hali yetu ya kukosa kukamilika. Na hata “kifo hakitakuwa tena.” Watu wenye wanamupenda Muumbaji wetu na kumutii, wataishi milele. Wataishi milele wapi?

Muumbaji Wetu Atageuza Hii Dunia Kuwa Paradiso

“Jangwa na inchi yenye kukauka vitafurahi, jangwa tambarare litashangilia na kutoa maua kama zafarani.”​—ISAYA 35:1.

Wakati Mungu atatosha mambo yote ya mubaya, dunia itakuwa paradiso! Mu dunia mutakuwa mabustani ya mingi ya muzuri na kutakuwa chakula ya mingi. (Zaburi 72:16) Bahari na mitoni itakuwa na maji yenye kuwa safi. Na mu ile maji mutakuwa viumbe mingi vyenye kuwa na uzima. Watu hawatakumbuka tena kama dunia ilikuwaka buchafu. Watu wataishi mu manyumba yenye wao wenyewe walijijengea. Hakuna tena mutu mwenye atakosaka nyumba, mwenye atakuwaka na njaa, ao mwenye atakuwaka maskini.​—Isaya 65:21, 22.

Mungu Atafufula Wafu

“Kutakuwa ufufuo.”​—MATENDO 24:15.

Utapenda kuona tena wapendwa wako wenye walishakufa? Mungu Mweza-Yote atawapatia tena uzima, ni kusema, atawafufula na wataishi mu paradiso hapa ku dunia. Utawajua na wao watakujua. Wazia namna mutafurahi wakati mutaonana tena! Juu ya nini tuko hakika kama ile jambo itatimia kabisa? Ni juu Biblia inatutolea mifano ya watu wakubwa na watoto wenye walifufuliwaka, na wakaonana tena na watu wa familia yao. Zaidi ya ile, mara mingi Yesu alifufua watu mbele ya mashahidi wengi.​—Luka 8:49-56; Yohana 11:11-14, 38-44.