Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SEHEMU YA KUULIZA MAULIZO | RAJESH KALARIA

Mwanasayansi wa Magonjwa ya Ubongo Anafasiria Imani Yake

Mwanasayansi wa Magonjwa ya Ubongo Anafasiria Imani Yake

PROFESA Rajesh Kalaria, wa Masomo ya Juu ya Newcastle, katika Uingereza, alijifunza ubongo wa mwanadamu kwa zaidi ya miaka 40. Alikuwa mwenye kuamini mageuzi. Lakini, alibadilisha mawazo yake. Amuka! ilimuuliza maulizo kuhusu kazi na imani yake.

Tafazali, utuambie kama ulikomalia katika dini gani.

Baba yangu alizaliwa India, na mama yangu, hata kama alikuwa wa asili ya India, alizaliwa Uganda. Maisha yao yaliongozwa zaidi sana na desturi ya Wahindu. Tulizaliwa watoto tatu na mimi ni wa pili. Tuliishi Nairobi, Kenya. Wahindu wengine wengi waliishi karibu na kwetu.

Ni nini ilifanya upendezwe na sayansi?

Nilipendezwa sana na wanyama, na nilizoea kufanya matembezi na kupiga kambi pamoja na marafiki zangu ili kufurahia wanyama na mimea katika pori. Kusudi langu la kwanza lilikuwa kuwa munganga mwenye kufanya upasuaji wa wanyama. Lakini, kisha kumaliza masomo huko Nairobi, nilienda Uingereza ili kujifunza magonjwa kwenye Masomo ya Juu ya Londres. Kisha, nilifanya utafiti kuhusu ubongo wa mwanadamu.

Mambo yenye ulijifunza yalikuwa na matokeo juu ya imani yako?

Ndiyo. Kadiri nilijifunza sayansi, niliona kuwa vigumu kuamini habari za kutunga na desturi za Wahindu, kama vile kuabudu wanyama na sanamu.

Sababu gani ulikubali fundisho la mageuzi?

Wakati nilikuwa mudogo, watu wengi wenye tuliishi nao waliamini kwamba mageuzi ya mwanadamu yalianza Afrika, na mara nyingi tulizungumuzia jambo hilo kwenye masomo. Tena, walimu na maprofesa wa masomo ya juu walitufanya, sisi wanafunzi, tufikiri kwamba wanasayansi wote wenye kujulikana wanaamini mageuzi.

Kisha wakati fulani, ulifikiria tena habari kuhusu chanzo cha uzima. Sababu gani?

Nilikuwa nikijifunza biolojia na anatomia kwa miaka fulani wakati mwanafunzi mwenzangu aliniambia mambo yenye alikuwa anajifunza kuhusu Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Nilipenda kujua mambo zaidi. Kwa hiyo, wakati Mashahidi wa Yehova walifanya mukusanyiko kwenye masomo yetu huko Nairobi, nilikusanyika pamoja nao. Kisha, misionere wawili Mashahidi wa Yehova walinifasiria mafundisho fulani ya Biblia. Imani yao katika Muumbaji Mukubwa mwenye anatoa majibu kwa maulizo ya maana katika maisha haikuwa kama hadisi za kutunga. Kwangu, imani yao ilionekana kuwa yenye kupatana na akili.

Ujuzi wako wa mambo ya kinganga ulikuzuia kuwa na imani katika uumbaji?

Hapana! Kadiri nilijifunza anatomia, niliona namna gani viumbe vyenye kuishi viliumbwa kwa njia ya ajabu. Kulingana na mawazo yangu, kusema kwamba vitu hivyo vya ajabu vilitokea kwa aksidenti, hakupatane na akili.

Unaweza kutupatia mufano?

Nilianza kujifunza ubongo wa mwanadamu tangu mwaka wa 1971, na kiungo hicho cha ajabu kinaendelea kunishangaza. Ubongo ndio chanzo cha mawazo na kumbukumbu, na unaongoza mambo mengi yenye kutendeka katika mwili. Uwezo mbalimbali wa mwili wetu unaongozwa na ubongo, na ubongo huo unaelewa habari kutoka ndani na inje ya mwili.

Ubongo wetu unafanya kazi muzuri hivyo zaidi sana kwa sababu ya kemia yake ya ajabu na chembe za neva zenye kufanya kazi ambazo ni chembe za musingi za ubongo. Ubongo wa mwanadamu uko na mamiliare mingi ya chembe za neva zenye kupashana habari kupitia nyuzi ndogo-ndogo na ndefu zenye kuitwa aksoni. Kupitia aksoni hizo, kila moja ya chembe ya neva inaungana na maelfu ya chembe zingine za neva kupitia nyuzi ndogo-ndogo zenye kuitwa dendira ambazo zinatoka kwenye chembe za neva. Matokeo ni kwamba hesabu kamili ya viunganishi katika ubongo ni kubwa sana! Zaidi ya hilo, chembe za neva hizo zote hazipangwe ovyoovyo, zinapangwa kwa utaratibu mukubwa sana. Ni muunganisho wenye kushangaza wa nyuzi.

Tafazali unaweza kufasiria?

Muunganisho huo wa nyuzi unaendelea kupangwa kwa utaratibu wakati mutoto anaendelea kukomaa katika tumbo la uzazi na pia kisha kuzaliwa. Chembe za neva zinatuma nyuzi kwenye chembe zingine za neva zenye zinaweza kuwa kwenye sentimetre fulani mbali​—huo ni umbali mukubwa kulingana na ukubwa wa chembe. Nafasi nyuzi inaenda, pengine haiko tu kwenye chembe fulani ya pekee, lakini kwenye sehemu fulani ya pekee ya chembe hiyo.

Wakati nyuzi mupya inatoka kwenye chembe ya neva, inaongozwa na alama za kikemia zenye kusema mambo kama vile “simama,” “enda,” ao “geuka” mupaka nyuzi hiyo itafika kwenye inaenda. Bila maagizo yenye kuwa wazi, nyuzi zenye kukomaa zitapotea haraka. Utaratibu huo wote unaongozwa kwa njia ya ajabu, na unaanza na maagizo yenye kuwa ndani ya ADN yetu.

Hata hivyo, tungali mbali sana ili kuelewa kabisa namna ubongo unakomaa na kufanya kazi, kutia ndani namna unatokeza kumbukumbuku, hisia, na mawazo. Kulingana na mimi, kujua tu kwamba ubongo unafanya kazi​—hata kama hatuzungumuzie sana namna unafanya kazi na namna unakomaa kwa njia yenye kupendeza​—kunaonyesha kwamba kuko mutu mwenye kuwa na akili ya juu kuliko yetu.

Sababu gani ulifikia kuwa Shahidi wa Yehova?

Mashahidi wa Yehova walinionyesha ushuhuda wa kwamba Biblia ni Neno la Mungu. Kwa mufano, Biblia haiko kitabu cha sayansi, lakini kila mara wakati inazungumuzia mambo ya sayansi haidanganyike. Tena, iko na unabii wa kweli. Inafanya pia maisha ya watu wenye kutumikisha mafundisho yake yakuwe muzuri. Maisha yangu mwenyewe yanashuhudia jambo hilo. Tangu nilikuwa Shahidi wa Yehova katika mwaka wa 1973, Biblia imekuwa kitabu chenye kuongoza maisha yangu. Matokeo ni kwamba nimekuwa na maisha mazuri kabisa na yenye kusudi.