Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna ya Kusamehe

Namna ya Kusamehe

MUSAADA KWA FAMILIA | NDOA

Namna ya Kusamehe

TATIZO

Wakati unabishana na bibi ao bwana yako, mara nyingi unafufua mambo mengi ya zamani, kwa kurudilia matatizo ya wakati uliopita ambayo yangetatuliwa wakati huo. Tatizo ni gani? Labda mumoja kati yenu ao ninyi wote wawili hamujue namna ya kusamehe.

Unaweza kujifunza kusamehe. Hata hivyo, fikiria sababu gani inaweza kuwa vigumu kwa bibi na bwana kusameheana.

SABABU GANI JAMBO HILO LINATOKEA?

Mamlaka. Bibi na bwana fulani wanakataa kusamehe ili kuendelea kuwa na mamlaka juu ya bibi ao bwana zao. Kwa hiyo, wakati tatizo linatokea, wanatumia jambo lililotokea wakati uliopita ili kujionyesha kuwa wenye mamlaka juu ya bibi ao bwana zao.

Kinyongo. Mutu anapoumizwa moyoni anaweza kufanya siku nyingi ili ajisikie vizuri. Bibi ao bwana anaweza kusema, ‘Ninakusamehe’ lakini anaendelea kuweka kinyongo kwa sababu ya jambo ambalo lilitokea, na labda anaweza hata kutamani kulipiza kisasi.

Kuvunjika moyo. Watu fulani wanafunga ndoa wakiamini kabisa kwamba maisha yataendelea kuwa ya raha tu sikuzote. Kwa hiyo, wakati wanakosa kuelewana, wanakataa kubadili maoni yao, wakijiuliza namna gani “bibi ao bwana ambaye waliwazia kuwa mukamilifu” anaweza kushindwa kuwaelewa. Kutazamia mambo yasiyo ya kweli kunaweza kumufanya mutu awe mwepesi zaidi kuona makosa na kutokuwa tayari kusamehe.

Kuelewa vibaya maana ya kusamehe. Bibi na bwana wengi wanakataa kusamehe kwa sababu wanaelewa vibaya ikiwa kusamehe kutamaanisha nini. Kwa mufano:

Ikiwa ninasamehe, nitapunguza uzito wa kosa.

Ikiwa ninasamehe, nitasahau jambo ambalo lilitokea.

Ikiwa ninasamehe, hilo litamufanya anitendee tena vibaya.

Kwa kweli, kusamehe hakumaanishe jambo lolote kati ya mambo hayo. Lakini, kusamehe linaweza kuwa jambo ngumu, zaidi sana katika uhusiano kati ya bibi na bwana.

MAMBO AMBAYO UNAWEZA KUFANYA

Uelewe maana ya kusamehe. Katika Biblia, wakati fulani neno “kusamehe” linamaanisha “kuacha.” Kwa hiyo, kusamehe hakumaanishe sikuzote kusahau jambo ambalo lilitokea ao kupunguza uzito wa kosa. Wakati fulani kunamaanisha kwamba unahitaji tu kuachilia mambo ili hali yako iwe nzuri na ili ndoa yako pia iwe katika hali nzuri.

Tambua matokeo mabaya ya kukosa kusamehe. Watu fulani wenye elimu wanasema kwamba kuweka kinyongo kunaweza kukuletea matatizo mengi ya kimwili na ya kimoyoni, kutia ndani kushuka moyo na kupanda sana kwa damu ndani ya mwili, na hilo linaweza pia kukuletea matatizo katika ndoa yako. Ndiyo sababu Biblia inasema hivi: ‘Iweni wenye fazili ninyi kwa ninyi, wenye huruma nyororo, mukisameheana kwa hiari.’​—Waefeso 4:32.

Tambua faida za kusamehe. Kuliko “kuweka hesabu ya mabaya,” roho ya kusamehe inakufanya wewe na bibi ao bwana yako kuwa na uhakika kwamba mwenzako hakuwa na nia mbaya wakati alikukosea. Na hilo linakusaidia kufanyiza hali ambayo itakuwezesha kuondoa kinyongo na hivyo kuruhusu upendo ukomae.​—Kanuni ya Biblia: Wakolosai 3:13.

Elewa mambo namna yalivyo. Ni rahisi sana kuwa mwenye kusamehe ikiwa unakubali hali ya bibi ao bwana yako, ijapokuwa uzaifu wake. Kitabu kimoja kinasema hivi: “Ikiwa unakazia akili makosa ya bibi ao bwana yako, ni vyepesi sana kusahau sifa zake nzuri. Ni mambo gani ambayo unataka kukazia akili katika maisha yako?” (Fighting for Your Marriage) Kumbuka kwamba hakuna mutu mukamilifu, hata wewe pia.​—Kanuni ya Biblia: Yakobo 3:2.

Uwe mwenye usawaziko. Wakati bibi ao bwana yako atakukosea kwa kufanya ao kusema jambo fulani, ujiulize hivi: ‘Je, jambo hilo ni kosa kabisa? Je, ninahitaji kungojea bibi ao bwana yangu aniombe musamaha, ao ninaweza tu kusahau jambo ambalo lilitokea na kuendelea na maisha?’​—Kanuni ya Biblia: 1 Petro 4:8.

Ikiwa ni lazima, muzungumuzie tatizo. Eleza kwa upole jambo ambalo lilikuumiza moyoni na sababu gani jambo hilo lilikufanya ujisikie vibaya. Usimuwazie bibi ao bwana yako vibaya wala kusema maneno yenye kuonyesha kwamba unashikilia tu mawazo yako, kwa sababu hilo litamufanya bibi ao bwana yako ajitetee. Kuliko kufanya hivyo, eleza tu sababu gani mambo ambayo bibi ao bwana yako alifanya yalikuumiza moyoni.