Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 MAMBO YENYE HISTORIA INATUFUNDISHA

William Whiston

William Whiston

William Whiston alikuwa mwanasayansi, mwenye elimu ya hesabu, alikuwa kiongozi wa dini, aliandika vitabu vingi, na alifanya kazi pamoja na mwanafizikia Mwingereza na mwenye elimu ya hesabu, Sir Isaac Newton. Katika mwaka wa 1702, Whiston alichukua nafasi ya Newton na kuwa Profesa wa Hesabu kwenye Masomo ya Juu ya Cambridge, Uingereza. Watu ambao walikuwa na akili nyingi sana katika mambo ya sayansi na teknolojia ndio walikuwa wanapata cheo hicho.

WHISTON anajulikana pia, zaidi sana na Wanafunzi wa Biblia, kwa sababu alitafsiri katika Kiingereza maandishi ya Flavius Josèphe, ambaye ni mwanahistoria Muyahudi aliyeishi wakati mitume. Maandishi ya Josèphe yanafunua mambo mengi juu ya historia ya Wayahudi na hali ambamo Wakristo wa kwanza waliishi.

MAMBO AMBAYO WHISTON ALIAMINI

Whiston alikuwa na akili nyingi na alijifunza mambo mengi, zaidi sana mambo ya sayansi na dini. Aliamini kwamba masimulizi ya Biblia juu ya uumbaji ni ya kweli na kwamba namna vitu vimefanywa kwa njia ya ajabu, nzuri, na yenye utaratibu inaonyesha kwamba kuna Muumbaji.

Pia, Whiston aliamini kwamba dini zinazojiita kuwa za Kikristo zimegawanyika kwa sehemu nyingi kwa sababu viongozi wa dini hizo hawafuate Biblia, wanapendelea mafundisho yasiyo katika Biblia na mapokeo ya mabaraza ya kanisa na ya wale wanaoitwa eti Mababa wa Kanisa.

Kwa sababu aliamini kwamba Biblia ni kitabu kinachofundisha kweli juu ya Mungu, Whiston alikataa fundisho la kuteswa milele katika moto. Aliona fundisho hilo kuwa lisilopatana na akili na lenye kumufanya Mungu aonekane kuwa mukali, na pia linamupunguzia heshima. Lakini, hakusikilizana na viongozi wa kanisa zaidi sana kwa sababu alikataa kuamini Utatu, fundisho linaloonyesha kwamba katika Mungu mumoja kuna watu watatu walio na uwezo uleule na wote ni wa milele, ni kusema, Baba, Mwana, na Roho Takatifu. Hata hivyo, inasemekana kwamba hakuna miungu tatu, lakini mungu mumoja.

 “ALIFUKUZWA KWENYE MASOMO YENYE KUJULIKANA SANA”

Kisha kuchunguza mambo kwa uangalifu, Whiston alitambua kwamba Wakristo wa kwanza hawakufundisha Utatu lakini ulikubaliwa wakati filozofia ya wapagani iliingia katika dini ya Kikristo. * Marafiki wake walimuonya kuhusu hatari ya kutangaza mambo aliyovumbua, lakini Whiston hangeweza kunyamazia mambo aliyotambua kuwa uongo kuhusu namna Yesu alivyo kabisa. Aliamini kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu, aliyeumbwa na Mungu.

Masomo ya juu ya Cambridge ilifukuza mutu yeyote aliyefundisha mambo yaliyokuwa tofauti na mafundisho ya kanisa la Kianglikani; hilo lilimaanisha kwamba Whiston angepoteza cheo chake. Hata hivyo, hakunyamaza kama Newton, ambaye pia aliona Utatu kuwa fundisho la uongo lakini aliogopa kueleza mawazo yake. Whiston aliandika: “Hakuna jambo lolote ambalo litanidanganya.”

Kwa sababu alishikamana na mambo aliyoamini, Whiston “alifukuzwa kwenye masomo yenye kujulikana sana”

Katika mwaka wa 1710, Whiston alifukuzwa kwenye Masomo ya Juu ya Cambridge. Alifukuzwa kwenye masomo yenye kujulikana sana,” kwa sababu alishikamana na imani yake. Hata hivyo, hilo halikumuogopesha. Wakati alishitakiwa kuwa muasi-imani, aliandika vitabu vilivyoitwa La renaissance du christianisme primitif; neno la Kifaransa “primitif” linamaanisha Ukristo wa mwanzoni, uliofuatwa na wafuasi wa kwanza wa Yesu. Baadaye, Whiston alianzisha Kikundi cha Kutetea Ukristo wa Mwanzoni, na watu waliokuwa katika kikundi hicho walikuwa wanafanya mikutano yao kwake, huko Londres.

Hata ikiwa alipoteza cheo chake na kuwa na matatizo ya kupata feza kwa muda fulani, Whiston aliendelea kuandika na kutetea imani yake katika nyumba ambamo watu walienda kunywa kahawa huko Londres. Katika mwaka wa 1737, alichapisha tafsiri yake ya maandishi ya Josèphe ili kusaidia watu waelewe namna maisha yalikuwa wakati Ukristo ulianza. Tangu wakati huo tafsiri hiyo imeendelea kuchapishwa.

Mwandikaji James E. Forcean anasema kwamba watu wengi leo wanamuona Whiston kuwa “mutu wa pekee sana” kwa sababu alionyesha ujasiri wake hata ikiwa watu wengi hawakumupenda. Lakini wengine wanamufurahia kwa sababu alichunguza sana Biblia, alitafuta sana kujua ukweli juu ya dini, na alikuwa mutu aliyeazimia kuishi kulingana na mambo aliyoamini.

^ fu. 10 Biblia inaeleza waziwazi namna Mungu alivyo. Ili kupata habari zaidi, fungua adresi yetu ya internete jw.org. Soma chini ya MAFUNDISHO YA BIBLIA> MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA.

[Sanduku katika ukurasa wa 12]