Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 KITU HIKI KILIJIFANYA CHENYEWE?

Muguu wa Farasi

Muguu wa Farasi

FARASI (Equus caballus) anaweza kukimbia kilometa 50 kwa saa. Hata ikiwa hilo linaomba kazi nyingi ya viungo, lakini anatumia nguvu kidogo. Namna gani jambo hili linawezekana? Siri yake inapatikana katika miguu yake.

Fikiria jambo linalotokea wakati farasi anakimbia. Mishipa iliyo katika nyama ya miguu inafyonza nguvu wakati farasi anakanyanga chini, na kama vile kamba ya chuma inayonepanepa, mishipa inarudisha nguvu hiyo, na hilo linafanya farasi aende mbele.

Zaidi ya hilo, anapokimbia, miguu yake inatetemeka hivi kwamba mishipa iliyo katika nyama ya miguu inaweza kuregea. Lakini, nyama ya miguu inazuia jambo hilo. Wachunguzi wanasema hiyo ni “mishipa ya nyama ya miguu ya hali ya juu” ambayo inatoa nguvu na uwezo wa kukimbia haraka.

Mafundi wanajikaza kuiga namna miguu ya farasi imeumbwa wanapotengeneza roboti zenye miguu ine. Lakini, kulingana na Biomimetic Robotics Laboratory of the Massachusetts Institute of Technology, vitu na ufundi tulio nao sasa hauwezi kutuwezesha kuiga kwa urahisi namna miguu ya farasi imeumbwa.

Unawaza nini? Miguu ya farasi ilitokana na mageuzi ao iliumbwa?