Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA

Tumaini kwa Wasio na Makao na kwa Masikini

Tumaini kwa Wasio na Makao na kwa Masikini

Joe alikuwa askari katika jeshi la Amerika. Matatizo yake mwenyewe na ya familia yake yalimufanya abakie bila makao kwa miaka 18 hivi. Wakati fulani alianza kutembelea chumba cha vitabu katika eneo lake, na mara nyingi alizungumuza na mwanamuke mumoja aliyetumika mahali hapo. Mazungumuzo hayo yalibadilisha maisha yake.

Kijana mumoja mwanaume anayeitwa Martín wa inchi ya Argentine, alijisikia kuwa mbali na Mungu. Aliona kuwa maisha hayana maana. Aliondoka nyumbani ili kutafuta maana ya maisha, na mwishowe alianza kuishi pembeni ya bahari. Lakini kuliko kupata majibu yenye alikuwa anatafuta, alivunjika moyo sana. Alilia na kumuomba Mungu hivi: “Ikiwa uko kabisa, tafazali unisaidie nikupate.” Matokeo yalikuwa nini? Tutaona.

KUNA sababu mbalimbali zenye kufanya watu wabaki bila makao. Kwa watu fulani kama vile Joe, ni kwa sababu ya matatizo katika maisha yao wenyewe. Wengine kama vile Martín, wanachagua tu kuacha maisha ya kawaida, na wanaona kuwa hayana maana. Na wengine wanabaki bila makao kwa sababu ya umasikini, misiba ya asili, kutendewa mubaya nyumbani, kutumia dawa za kulewesha ao kunywa pombe kupita kiasi, magonjwa ya akili, kukosa nyumba ya bei chini, ao kwa sababu ya kupoteza kazi.

Zamani watu waliwaza kama tatizo la kukosa makao linaonekana tu katika inchi masikini ao zenye kuwa na vita ao matatizo ya feza. Lakini Profesa Paul Toro mwenye kujifunza tabia za watu, alisema kuwa hilo “limekuwa tatizo kubwa hata katika inchi nyingi tajiri.” * Inawezekana kati ya sababu zenye zinafanya hali ikuwe hivyo, ni kwamba serikali hazigawanye muzuri misaada yenye kupewa familia masikini, na pia matajiri wanaendelea kuwa matajiri sana na masikini wanaendelea kuwa masikini sana.

Watu wengi wanahangaika juu ya wakati unaokuja. Lakini watu fulani wamepunguza mahangaiko yao kwa kujifunza mambo yenye Biblia inasema juu ya wakati unaokuja; tutazungumuzia mambo hayo. Biblia inaweza kutusaidia leo kwa kutupatia kanuni zenye tunapaswa kufuata katika maisha yetu. Kanuni hizo zinaweza kutusaidia kupunguza mahangaiko juu ya feza, na kuwa na amani ya akili; Joe na Martín walijionea jambo hilo.

BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YAKE

Cindi alikuwa anatumika katika chumba cha vitabu na mara kwa mara alimuona Joe mahali hapo. Alisema hivi: “Joe alionekana kuwa mwenye akili, mwenye adabu, na munyenyekevu.” Kwa sababu Cindi ni Shahidi wa Yehova, alimupatia Joe magazeti Munara wa Mulinzi na Amuka! Pia alimualika kwenye mukutano wa Kikristo. Kwenye mukutano huo, alitendewa kwa upendo na kwa heshima. Kwa hiyo alianza kufika kwenye mikutano kila juma. Pia alikubali wakati Shahidi mumoja mwanaume alimuambia ataanza kumufundisha Biblia.

Funzo la Biblia lilimusaidia Joe kuwa na maisha yenye kumuletea heshima

Joe alitiwa moyo sana na mambo yenye alijifunza, na alianza kutumikisha mafundisho ya Biblia, hata kama hilo lilimuomba afanye mabadiliko makubwa katika maisha yake. Kwa mufano, alijifunza kuwa uzima ni zawadi kutoka kwa Mungu na unapaswa kuheshimiwa, na kuwa tumbaku inachafua mwili. (Zaburi 36:9) Kwa hiyo aliacha kuvuta, ili kutii kanuni hii yenye kuwa katika andiko la 2 Wakorintho 7:1: “Acheni tujisafishe wenyewe kila unajisi [uchafu] wa mwili.” Bila shaka, uamuzi wa Joe ulimusaidia kuwa na afya ya muzuri na ulimusaidia kutumia vizuri feza zake.

Joe alipenda kutumikisha shauri la Biblia lenye kusema kuwa tunapaswa kufanya kazi ili kupata mambo yenye tuko nayo lazima, kwa hiyo alianza kutafuta kazi. * (1 Wathesalonike 4:11, 12) Andiko la Mhubiri 2:24 linasema hivi: ‘Kwa mwanadamu hakuna jambo bora kuliko kwamba akule, na akunywe na kuifanya nafsi yake ione mema kwa sababu ya kazi yake.’ Mutu anapata furaha hiyo wakati anaishi maisha yenye kumuletea heshima, kwa sababu kazi nzuri inatuletea heshima. Pia inatuwezesha kusaidia watu wenye kuwa na lazima ya musaada.—Waefeso 4:28.

Mashahidi waliona kuwa Joe alipenda kabisa kubadilisha maisha yake. Cindi anasema hivi: “Mashahidi walimukaribisha kwa furaha na wakamusaidia kupata nyumba ya muzuri na vitu vingine vyenye alikuwa na uwezo wa kupata.” Joe aliendelea kufanya maendeleo, na kisha wakati fulani alibatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova. Kwa sababu ya mambo yenye amejionea, anaweza kutia wengine moyo watafute hekima ya Mungu inayopatikana katika Biblia.—Methali 3:13, 14.

ALIFIKIA KUJUA MAANA YA MAISHA

Martín alianza kutafuta maana ya maisha wakati alikuwa na miaka 20. Anasema hivi: “Nilichunguza dini mbalimbali na filozofia, na nilitumia dawa za kulewesha ili nipate mambo yenye nilijisikia kuwa ninakosewa moyoni, lakini sikuyapata.” Aliishi California, Amerika kwa wakati fulani, kisha akahamia Hawaii. Martín anakumbuka hivi: “Niliwaza kama nimepata paradiso.” Lakini kuishi katika muji wenye kupendeza haikufanya apate mambo yenye alikuwa anakosewa moyoni. Tena anakumbuka hivi: “Nilivunjika moyo sana, na hata nikapanga kujiua.” Katika maisha yake ni wakati huo ndio alilia sana na kumuomba Mungu hivi: “Ikiwa uko kabisa, tafazali unisaidie nikupate.”

Leo Martín iko na mawazo mazuri juu ya maisha

Martín alikumbuka kama zamani alisoma maneno haya mahali fulani: “Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova.” Aliamua kuenda mahali hapo kwenye mukutano wa Kikristo. Alisema hivi: “Wakati niliingia ndani, nilikuwa na ndevu na nywele nyingi, na nilikuwa ninavaa nguo zenye nilivaa tangu miezi mingi. Lakini, walinikaribisha kwa furaha.” Martín alikubali kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova na kila mara alikuwa anatoka “nyumbani” kwake, ni kusema, pembeni ya bahari na kuenda katika muji ili kujifunza.

Mwishowe, Martín alianza kupata majibu yenye kusadikisha kwa maulizo yake. Matokeo ni kwamba, hakukuwa tena mwenye kuvunjika moyo, na alipata furaha yenye Yesu alizungumuzia wakati alisema: “Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji wao wa kiroho.”—Mathayo 5:3.

“Watu walishangaa kuona mabadiliko yenye nilikuwa ninafanya”

Martín alianza kuwa na mawazo mazuri juu ya maisha, na hilo lilionekana wakati alianza kutumikisha kanuni za Biblia zenye zilisaidia pia Joe kutengeneza na kuongoza maisha yake. Martín alianza kuhangaikia sura yake na kuvaa vizuri, na Mashahidi wa Yehova walimusaidia kupata kazi na mahali pa kuishi. Alisema hivi: “Zamani, watu wa eneo langu walinijua kuwa mutu asiye na makao, lakini sasa watu walishangaa kuona mabadiliko yenye nilikuwa ninafanya.”

Baada ya muda, Martín alirudi Argentine, na huko alibatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova. Sasa anafurahia pendeleo la kusaidia wengine wenye kuwa na njaa ya kiroho, kupata majibu ya maulizo ya lazima juu ya maisha.

WAKATI WATU HAWATAKOSA TENA MAKAO NA HAWATAKUWA TENA MASIKINI

Yeremia, mutumishi wa zamani wa Yehova, aliishi katika kipindi kigumu sana. Maadui wasio na huruma walishambulia muji wake na kupeleka wakaaji wengi katika inchi ya mbali na kuwafanya kuwa watumwa. (Maombolezo 1:3) Maadui hao hawakubeba Yeremia lakini alipoteza karibu kila kitu. Alisali hivi kwa uchungu: “Ukumbuke mateso yangu na hali yangu ya kukosa makao.”—Maombolezo 3:19.

Yeremia hakukata tumaini hata kama alipata mateso mengi. Sababu gani? Kwa sababu alijua kama Yehova hawezi kumuacha. (Yeremia 1:8) Tena alijifunza katika Maandiko kama kuna siku hakutakuwa tena umasikini na mateso, lakini kutakuwa amani ya kweli na usalama.—Zaburi 37:10, 11.

Haiko wanadamu ndio wataleta hali hizo lakini zitaletwa na serikali kamilifu yenye inaitwa Ufalme wa Mungu. (Danieli 7:13, 14) Mufalme wa Ufalme huo ni Yesu Kristo. Wakati alikuwa mwanadamu hapa duniani, alionyesha huruma kubwa kwa masikini. (Luka 7:22; 14:13) Wakati wa utawala wake, ‘mwadilifu atachipuka na wingi wa amani . . . Atamukomboa masikini anayelilia musaada, pia mwenye kuteseka na yeyote ambaye hana musaidizi. Ataikomboa nafsi yao kutoka katika ukandamizaji na katika jeuri.’—Zaburi 72:7, 12, 14.

“Watajenga nyumba na kukaa ndani yake.”—Isaya 65:21

Wakati Yesu alikuwa anafundisha, alikazia sana Ufalme wa Mungu. (Luka 4:43) Hata alifundisha watu kusali hivi: ‘Ufalme wako uje. Mapenzi yako yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.’ (Mathayo 6:9, 10) Maisha yatakuwa namna gani wakati Ufalme wa Mungu utatawala dunia? Biblia inatuambia mbele ya wakati mambo mazuri ya wakati huo. Kwa mufano, inasema hivi juu ya watu wenye watatawaliwa na Ufalme wa Mungu:

  • ‘Hakika wao watajenga nyumba na kukaa ndani yake; na hakika wao watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake. Hawatajenga na mutu mwingine akae ndani yake; hawatapanda na mutu mwingine akule. . . . Watu wangu waliochaguliwa wataitumia kazi ya mikono yao wenyewe kikamilifu.’Isaya 65:21, 22.

  • ‘Wataketi, kila mutu chini ya muzabibu wake na chini ya mutini wake, wala hakutakuwa na mutu yeyote anayewatetemesha; kwa maana kinywa cha Yehova wa majeshi kimesema hivyo.’Mika 4:4.

Tumaini hilo la hakika linaweza kututia moyo wakati tunapambana na magumu. Pia, kanuni za Biblia zinaweza kutusaidia hata leo kuishi maisha yenye maana na yenye kufurahisha, kama vile Joe, Martín, na wengine wengi wamejionea. Bila shaka, Yehova Mungu, Muumbaji wetu anatuhakikishia hivi: ‘Mutu anayenisikiliza, yeye atakaa salama wala hatasumbuliwa na hofu [woga] ya musiba.’ (Methali 1:33) Maneno hayo na yatimie katika maisha yako!

^ fu. 6 Kwa sababu ya vita, jeuri, ao mateso, watu wengi sana wamelazimika kuacha nyumba zao ili kukimbilia katika inchi zingine, ao wamekuwa wenye kuhama-hama katika inchi yao. Tatizo hilo lilizungumuziwa katika gazeti Amuka! la tarehe 22 Mwezi wa 1, 2002.

^ fu. 11 Watu fulani wanapenda kufanya kazi, lakini hawawezi kufanya hivyo pengine kwa sababu ya ulemavu fulani, ugonjwa ao uzee. Mungu hapendi watu wenye ‘hawataki kufanya kazi.”—2 Wathesalonike 3:10.