Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KITU HIKI KILIJIFANYA CHENYEWE?

Uwezo wa Mwili Wetu wa Kuponyesha Vidonda

Uwezo wa Mwili Wetu wa Kuponyesha Vidonda

KATI ya utendaji mbalimbali wenye kufanya uzima wa mutu uwezekane, kuko uwezo wa mwili wa kuponyesha vidonda na kufanya upya chembe zenye ziliharibika. Uponyeshaji wa vidonda unaanza tu wakati mutu anaumia.

Fikiria hili: Uponyeshaji huo unawezekana kupitia utendaji mwingi wa chembe wenye kuwa mugumu kueleweka:

  • Chembe fulani zenye kugandisha damu ao kufanya damu ikamatane zinajiunga na chembe zingine kuzunguka kidonda, zinagandisha damu na zinafunga mishipa ya damu yenye iliharibika.

  • Kuvimba kunalinda kidonda ili kisiambukizwe na kunaondoa “uchafu” wowote wenye ulitokezwa kwa sababu ya kuumia.

  • Kisha siku fulani, mwili unaanza kubadilisha chembe zenye ziliharibika, unafanya kidonda kikokotane, na unatengeneza mishipa ya damu yenye iliharibika.

  • Mwishowe, chembe za kovu (alama yenye kubakia kisha kidonda kupona) zinatengeneza sehemu iliyoharibika na kuifanya kuwa nguvu.

Kwa kuiga namna damu inajigandisha, wachunguzi wako wanatengeneza vitu vya plastiki vyenye vinaweza “kujiponyesha” kama vinaharibika. Vitu kama hivyo vya kujiponyesha viko na mirija (tuyaux) mbili yenye kuwa na kemikali mbili ndani. Kemikali hizo zinaweza “kuvuja” wakati mirija inaharibika. Wakati kemikali hizo mbili zinachangana, zinafanyiza umajimaji fulani wenye kunata wenye unaingia nafasi zenye kuharibika, na unafunika mashimo na mahali penye kuchubuka. Umajimaji huo unapokuwa nguvu, unafanyiza kitu fulani chenye kuwa kigumu ambacho kinarudishia kitu hicho cha plastiki nguvu yake ya kwanza. Muchunguzi mumoja anaitika kama njia hiyo ya uponyeshaji yenye iko inatengenezwa “inafanana” na ile yenye kuwa tayari katika uumbaji.

Unawaza namna gani? Uwezo wa mwili wetu wa kuponyesha vidonda ulijifanya wenyewe? Ao uliumbwa?