Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Wakati wa zamani, wasimamizi-nyumba walikuwa na daraka gani?

WAKATI wa zamani, musimamizi-nyumba alikuwa anasimamia nyumba ao mali ya mutu mwingine. Wakati fulani maneno ya Kiebrania na ya Kigiriki yenye kutafsiriwa “musimamizi-nyumba” inamaanisha mwangalizi.

Wakati Yosefu, mwana wa Yakobo, alikuwa mutumwa katika inchi ya Misri, alifanywa kuwa musimamizi-nyumba wa nyumba ya bwana wake. Kwa kweli, bwana wake Mumisri “akaacha kila kitu chenye kilikuwa chake katika mikono ya Yosefu.” (Mwa. 39:2-6) Kisha, wakati Yosefu alifikia kuwa mutawala mwenye nguvu katika inchi ya Misri, aliweka musimamizi-nyumba juu ya nyumba yake mwenyewe.​—Mwa. 44:4.

Wakati wa Yesu, mara mingi wenye mashamba walikuwa wanaishi katika miji mbali na mashamba yao. Kwa hiyo, wenye mashamba walikuwa wanaweka wasimamizi-nyumba ili wasimamie kazi ya kila siku ya watumishi wenye walikuwa wanatumika katika ile mashamba.

Ni mutu gani mwenye alistahili kuwa musimamizi-nyumba? Columella, mwandishi mumoja Muroma wa wakati mitume, alionyesha kama mutumwa mwenye aliwekwa kuwa mwangalizi, ao musimamizi-nyumba, alipaswa kuwa “mutu mwenye alikuwa amepata uzoefu.” Musimamizi-nyumba alipaswa kuwa mutu mwenye “alihakikisha kama wafanyakazi wanafanya kazi yao na hakupaswa kuwa mukali.” Alisema pia kama jambo la maana zaidi lenye musimamizi-nyumba aliombwa ni hili: hakupaswa kuwaza kama anajua mambo yote na sikuzote alipaswa kuwa na hamu ya kujifunza mambo ya mupya.

Neno la Mungu linatumia mufano wa musimamizi-nyumba na kazi yake ili kuzungumuzia kazi fulani zenye kufanywa katika kutaniko la Kikristo. Kwa mufano, mutume Petro alitia moyo Wakristo watumie uwezo wenye Mungu aliwapatia “ili kutumikiana kama wasimamizi-nyumba wazuri wa fazili zenye hazistahiliwe za Mungu.”​—1 Pe. 4:10.

Yesu mwenyewe alizungumuzia musimamizi-nyumba katika mufano wake wenye kupatikana katika Luka 16:1-8. Tena, katika unabii fulani wenye alitoa juu ya alama yenye ingeonyesha kama amekuwa Mufalme, Yesu alihakikishia wanafunzi wake kama angeweka “mutumwa muaminifu na mwenye busara,” ao “musimamizi-nyumba muaminifu.” Kazi kubwa ya ule musimamizi-nyumba ni kupatia chakula cha kiroho wanafunzi wa Kristo katika wakati wa mwisho. (Mt. 24:45-47; Lu. 12:42) Tuko wenye shukrani kwa sababu tunapata vichapo vyenye kutia nguvu imani yetu vyenye ule musimamizi-nyumba muaminifu anatayarisha na kugawanya katika dunia yote.