Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Wamasora walifanya kopi za Maandiko kwa uangalifu

HABARI KUBWA | BIBLIA ILIOKOKA NAMNA GANI?

Biblia Iliokoka Hata Kama Watu Walijaribu Kubadilisha Ujumbe Wake

Biblia Iliokoka Hata Kama Watu Walijaribu Kubadilisha Ujumbe Wake

HATARI: Biblia haikupotea hata kama kulikuwa hatari ya kuharibika na upinzani. Lakini, watafsiri na watu fulani wenye kufanya kopi walijaribu kubadilisha ujumbe wa Biblia. Wakati fulani, walijaribu kupatanisha Biblia na mafundisho yao kuliko kupatanisha mafundisho yao na Biblia. Tuchunguze mifano fulani:

  • Mahali pa kufanyia ibada: Kati ya mwaka wa 400 na 101 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, waandikaji wa Pantateki ya Wasamaria waliongeza kisha andiko la Kutoka 20:17 maneno “kwenye Mulima Gerizimu. Na hapo mutajenga mazabahu.” Kwa hiyo, Wasamaria walipenda watu waamini kwamba Maandiko yanaunga mukono kujenga hekalu kwenye Mulima Gerizimu.

  • Fundisho la utatu: Karibu miaka 300 kisha kumaliza kuandika Biblia, muandikaji mumoja mwenye kuunga mukono fundisho la utatu aliongeza kwenye 1 Yohana 5:7 maneno “mbinguni, Baba, Neno na Roho Mtakatifu, na watatu hawa ni moja.” Maneno hayo hayakupatikana katika maandishi ya kwanza ya Biblia. Bruce Metzger, mutu mwenye elimu ya Biblia, anasema kwamba “kuanzia mwaka wa 501 na kuendelea,” maneno hayo “yalipatikana mara kwa mara katika maandishi ya Kilatini cha Zamani na katika Vulgate [ya Kilatini].”

  • Jina la Mungu: Kwa kufuata desturi ya Wayahudi ya kukataa kutaja jina la Mungu, watafsiri wengi wa Biblia waliamua kuondoa jina la Mungu katika Maandiko. Walibadilisha jina la Mungu na majina ya cheo kama vile “Mungu” ao “Bwana.” Lakini katika Biblia, majina hayo yanatumiwa ili kuzungumuzia Muumbaji, wanadamu, vitu vyenye kutumiwa katika ibada ya uongo, na hata Shetani.—Yohana 10:34, 35; 1 Wakorintho 8:5, 6; 2 Wakorintho 4:4. *

NAMNA BIBLIA ILIOKOKA: Kwanza, hata kama watu fulani wenye walifanya kopi za maandishi ya Biblia hawakuwa waangalifu ao hata kudanganya, wengine wengi walikuwa wenye ufundi na waangalifu sana. Wamasora walifanya kopi za Maandiko ya Kiebrania kati ya mwaka wa 501 na 1000 kisha kuzaliwa kwa Yesu. Kopi hizo zinaitwa Maandishi ya Wamasora. Inasemekana kwamba Wamasora walihesabu maneno na herufi ili kuhakikisha kama maandishi hayo hayana makosa. Kila nafasi waliwazia kwamba kulikuwa makosa katika maandishi yenye walitumia, waliandika pembeni. Wamasora walikataa kubadilisha maandishi ya Biblia. Profesa Moshe Goshen-Gottstein aliandika hivi: “Waliona kama kuyabadilisha kimakusudi ingekuwa kosa kubwa sana kwao.”

Pili, maandishi mengi yenye kupatikana leo yanasaidia watu wenye elimu ya Biblia wavumbue makosa. Kwa mufano, viongozi wa dini walifundisha kwa miaka mingi kwamba tafsiri yao ya Biblia katika Kilatini haikuwa na makosa. Lakini, kwenye andiko la 1 Yohana 5:7, waliingiza makosa yenye tumetaja katika habari hii. Makosa hayo yaliingizwa hata katika Biblia ya Kiingereza yenye kupendwa sana ya King James Version! Lakini, wakati maandishi mengine yalivumbuliwa yalionyesha nini? Bruce Metzger aliandika hivi: “Maneno [yenye kuwa kwenye 1 Yohana 5:7] hayapatikane katika tafsiri zote za zamani (Kisiria, Kikoptiki, Kiarmenia, Kietiopia, Kiarabu, Kislavonia), isipokuwa tu katika tafsiri ya Kilatini.” Matokeo ni kwamba Biblia ya King James Version yenye iliandikwa upya na Biblia zingine ziliondoa makosa hayo.

Chester Beatty P46, funjo la maandishi ya Biblia ya tangu mwaka wa 200 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu.

Maandishi ya zamani yanashuhudia kwamba ujumbe wa Biblia haukubadilishwa? Wakati Vitabu vya Kukunjwa vya Bahari ya Chumvi vilivumbuliwa katika mwaka wa 1947, watu wenye elimu ya Biblia walilinganisha maandishi ya Kiebrania ya Wamasora na maandishi ya vitabu vya kukunjwa vya Biblia vyenye viliandikwa zaidi ya miaka elfu moja mbele. Mumoja kati ya watu wenye wanaandika habari juu ya Vitabu vya Kukunjwa vya Bahari ya Chumvi alisema kwamba kitabu kimoja kinatosha ili “kuhakikisha kabisa kwamba Wayahudi wenye walifanya kwa mikono kopi za maandishi ya Biblia kwa zaidi ya miaka elfu moja, walifanya hivyo kwa uaminifu na uangalifu sana.”

Maktaba ya Chester Beatty ya Dublin, Irlande, iko na mafunjo yenye kuwa na karibu kila kitabu cha Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Kati ya mafunjo hayo kuna yale yenye yaliandikwa kati ya mwaka wa 101 na 200, miaka 100 tu kisha kumaliza kuandika Biblia. Kitabu kimoja chenye kufasiria maneno ya Biblia kinasema hivi: “Hata kama mafunjo hayo yanaleta habari ya mupya juu ya maandishi, yanaonyesha pia kwamba ujumbe wa Biblia haukubadilika wakati watu walikuwa wanafanya kopi ya maandishi ya Biblia.”—The Anchor Bible Dictionary.

“Tunaweza kuhakikisha kwamba hakuna kitabu kingine cha zamani kimeandikwa hivyo bila makosa kutoka maandishi ya zamani”

MATOKEO: Kuliko kuingiza makosa katika Biblia, kupatikana kwa maandishi mengi ya Biblia na miaka yenye maandishi hayo yamefanya, kumesaidia ujumbe wa Biblia ukuwe muzuri zaidi. Frederic Kenyon aliandika hivi juu ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo: “Hakuna kitabu kingine cha zamani chenye kuwa na ushuhuda mwingi na wa zamani juu ya maandishi yake, na kila mutu mwenye elimu na mawazo ya muzuri anaweza kukubali kwamba maandishi yenye tuko nayo hayana makosa.” Na William Henry Green, mutu mwenye elimu alisema hivi juu ya Maandiko ya Kiebrania: “Tunaweza kuhakikisha kwamba hakuna kitabu kingine cha zamani kimeandikwa hivyo bila makosa kutoka maandishi ya zamani.”

^ fu. 6 Ili kupata habari zaidi, ona kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? kwenye ukurasa wa 195-197, kinapatikana pia kwenye adresi ya Internete www.mr1310.com.