Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Kuna siku tutakuwa na serikali moja katika dunia yote?

Namna Gani Serikali Moja Katika Dunia Yote Itaunganisha Watu wa Mataifa Yote? Isaya 32:1, 17; 54:13

Wazia namna serikali moja katika dunia yote inaweza kuletea watu faida. Leo watu wengi wanateseka kwa sababu wako maskini sana, wakati wengine ni matajiri sana. Lakini serikali moja katika dunia yote inayoelewa mambo watu wako nayo lazima inaweza kuhakikisha kuwa watu wote wanapata mambo hayo. Unawaza kuna siku watu watafanya serikali kama hiyo?​—Soma Yeremia 10:23.

Katika historia yote, serikali zimeshindwa katika njia nyingi kuhangaikia raia zake, zaidi sana maskini. Serikali fulani zinatesa watu. (Mhubiri 4:1; 8:9) Lakini Mungu Mweza-yote ameahidi kutuletea serikali itakayochukua nafasi ya serikali zingine zote. Mutawala wa serikali hiyo atahangaikia watu kabisa.​—Soma Isaya 11:4; Danieli 2:44.

Ufalme wa Mungu utafanya mambo gani?

Yehova Mungu amechagua Mutawala muzuri sana wa dunia; Mutawala huyo ni Mwana wake, Yesu. (Luka 1:31-33) Wakati alikuwa mwanadamu hapa duniani, Yesu alifurahia kusaidia watu. Akiwa Mufalme, ataunganisha watu wa mataifa yote na kuwaondolea mateso yote.​—Soma Zaburi 72:8, 12-14.

Kila mutu atamukubali Yesu kuwa Mutawala? Hapana. Lakini Yehova ni muvumilivu. (2 Petro 3:9) Amepatia watu nafasi ya kukubali Yesu kuwa Mutawala. Hivi karibuni, Yesu ataondoa watu wabaya katika dunia na kuleta amani na usalama katika dunia yote.​—Soma Mika 4:3, 4..