Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUENDELEE KUKESHA!

Mu Dunia Yote Muko Kifukutu Sana Kupita Kawaida​—Biblia Inasema Nini?

Mu Dunia Yote Muko Kifukutu Sana Kupita Kawaida​—Biblia Inasema Nini?

 Ripoti inaonyesha kama mu Mwezi wa 7, 2022, mu dunia yote mulikuwa kifukutu sana:

  •   “Kwa mara ya pili mu hii mwezi wakubwa wa serikali mu China wanaonya watu kama mu miji karibu 70 kutakuwa kifukutu yenye kuwa hatari sana.”—Tarehe 25, Mwezi wa 7, 2022, Kituo ya Habari ya CNN.

  •   “Juu mu Ulaya muko kifukutu yenye haiko ya kawaida, moto iko nalunguza mapori mu inchi mbalimbali.”—Tarehe 17, Mwezi wa 7, 2022, The Guardian.

  •   “Siku ya Yenga, miji mingi mu Amerika ilikuwa na kifukutu sana kupita wakati mwingine wowote, wakati kifukutu ya kipindi ya joto inaendelea mu maeneo ya Mashariki ya Pembeni ya Bahari na sehemu za Kusini na Mangaribi ya kati.”—Tarehe 24, Mwezi wa 7, 2022, The New York Times

 Ile yote inaonyesha nini? Kuko siku haitawezekana tena kuishi ku dunia? Biblia inasema nini?

Biblia ilitabiri hali ya hewa ya kifukutu sana?

 Ndiyo. Hali ya hewa ya kifukutu sana yenye iko mu dunia inapatana na mambo yenye Biblia ilitabiri juu ya wakati wetu. Kwa mufano, Yesu alitabiri kama tutaona “mambo yenye kuogopesha.” (Luka 21:11) Juu kifukutu inaongezeka sana mu dunia, watu wengi wanaogopa kama wanadamu wataharibu kabisa-kabisa dunia.

Kuko wakati haitawezekana tena kuishi ku dunia?

 Hapana. Mungu aliumba dunia juu ikaliwe na watu milele. (Zaburi 115:16; Muhubiri 1:4) Hataruhusu wanadamu waharibu dunia. Lakini ‘ataharibu wale wenye wanaharibu dunia’ sawa vile ameahidi.​—Ufunuo 11:18.

 Ona maunabii mbili tu yenye inaonyesha mambo ingine yenye Mungu ameahidi:

  •   “Jangwa na inchi yenye kukauka vitafurahi, jangwa tambarare litashangilia na kutoa maua kama zafarani.” (Isaya 35:1) Mungu hataacha dunia ikuwe jangwa yenye watu hawawezi kuishi ndani. Lakini atatengeneza sehemu za dunia zenye zimeharibika.

  •   “Unatunza dunia, unaifanya izae kwa wingi na kuifanya ikuwe tajiri sana.” (Zaburi 65:9) Mungu atabariki dunia na kuifanya kuwa paradiso.

 Ili kujua mambo mingi zaidi juu ya namna kubadilika kwa hali ya hewa kunatimiza unabii wa Biblia, soma habari “Biblia Inasema Nini juu ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Wakati Wetu Wenye Kuya?

 Ili kujua mambo mingi zaidi juu ya namna Mungu atatengeneza tena dunia, ona habari “Ni Nani Atakayeiokoa Dunia?