Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 14

Ni Masomo Gani Yenye Kutayarishwa kwa Ajili ya Mapainia?

Ni Masomo Gani Yenye Kutayarishwa kwa Ajili ya Mapainia?

Inchi ya Amerika

Masomo ya Gileadi, Patterson, New York

Panama

Kwa miaka mingi, masomo mbalimbali ya kiteokrasi imekuwa jambo la maana sana kwa Mashahidi wa Yehova. Wale wenye wanatumia wakati wao wote ili kufanya kazi ya kuhubiri Ufalme, wanapewa mazoezi ya pekee ili waweze ‘kutimiza kwa ukamili utumishi wao.’​—2 Timoteo 4:5.

Masomo ya Mapainia. Wakati painia wa kawaida anafanya mwaka moja katika utumishi wa wakati wote, anaalikwa kusoma masomo ya siku sita. Ile masomo inaweza kufanywa mu Jumba la Ufalme la karibu na kwao. Iko na kusudi la kusaidia painia amukaribie Yehova zaidi, akuwe na matokeo ya muzuri zaidi katika sehemu mbalimbali za kazi ya kuhubiri, na aendelee kufanya kazi ya upainia kwa uaminifu.

Masomo kwa Ajili ya Waeneza-Injili wa Ufalme. Ile masomo ya miezi mbili, iko na kusudi la kuzoeza mapainia wenye uzoefu wenye wanapenda kuenda kutumikia mahali kwenye kuko lazima kubwa ya wahubiri. Ni kama vile wanasema hivi: “Mimi huyu! Unitume mimi!” Wakati wanafanya vile, wanafuata mufano wa Yesu Kristo, Mweneza-Injili mukubwa zaidi, mwenye amekwisha kutumikia hapa ku dunia. (Isaya 6:8; Yohana 7:29) Kuhamia katika eneo la mbali, kunaweza kumuomba mutu aitike kuishi maisha mepesi zaidi. Pia, mambo kama vile desturi, hali ya hewa na chakula vinaweza kuwa tofauti kabisa na vyenye mutu alikuwa amezoea. Tena, inaweza kuomba mutu ajifunze luga ingine. Ile masomo inasaidia ndugu wenye hawajaoa, dada wenye hawajaolewa, na ndugu na dada wenye wamefunga ndoa, wenye kuwa na miaka 23 mupaka 65, wakomalishe sifa za kiroho zenye zitawasaidia mu mugao wao, na ufundi wenye utawasaidia wamutumikie Yehova na tengenezo lake kwa ukamili.

Masomo ya Biblia ya Gileadi. Mu Kiebrania neno “Gileadi” maana yake, “Rundo la Ushahidi.” Masomo ya Gileadi ilianzishwa mu mwaka wa 1943. Kuanzia mwaka huo, wamisionere zaidi ya 8 000 wenye wamesoma ile masomo, wametumwa ili kutoa ushahidi “kwenye miisho ya dunia,” na wamepata matokeo ya muzuri sana. (Matendo 13:47) Kwa mufano, wakati wamisionere walifika kwa mara ya kwanza mu inchi ya Peru, hakuna hata kutaniko moja lenye lilikuwa mu inchi hiyo. Lakini leo, kuko makutaniko zaidi ya 1 000. Wakati wamisionere walianza kutumikia mu inchi ya Japani, kulikuwa Mashahidi karibu 10. Lakini leo, kuko Mashahidi zaidi ya 200 000. Masomo ya Gileadi inafanya miezi tano, wakati huo ndugu na dada wanajifunza sana Neno la Mungu. Mapainia wa pekee, wamisionere wenye wanafanya kazi ya kuhubiri mu maeneo fulani, ndugu na dada wenye wanatumikia ku Beteli, na waangalizi wa muzunguko, wanaalikwa kusoma ile masomo. Wanapewa mazoezi yenye itawasaidia kufanya muzuri zaidi kazi ya kuhubiri mu dunia yote na kuitia nguvu.

  • Masomo ya Mapainia iko na kusudi gani?

  • Masomo kwa Ajili ya Waeneza-Injili wa Ufalme imetayarishwa kwa ajili ya nani?