Ona video zinazopatikana

Je, Mashahidi wa Yehova Wanafikiri Kama wao tu Ndio Wataokolewa?

Je, Mashahidi wa Yehova Wanafikiri Kama wao tu Ndio Wataokolewa?

 Hapana. Mamilioni ya watu walioishi zamani na ambao hawakuwa Mashahidi wa Yehova watapewa nafasi ya kuokolewa. Biblia inaonyesha kwamba katika ulimwengu mupya ambao Mungu aliahidi, “kutakuwa na ufufuo wa waadilifu na wasio waadilifu pia.” (Matendo 24:15) Vilevile, watu wengi wanaoishi sasa wanaweza kuamua kumutumikia Mungu ili waokolewe. Kwa vyovyote, si kazi yetu kuamua ni nani atakayeokolewa ao ni nani ambaye hataokolewa. Yesu ndiye amepewa kazi hiyo.—Yohana 5:22, 27.