Ona video zinazopatikana

Mashahidi wa Yehova Wanakubali Matunzo?

Mashahidi wa Yehova Wanakubali Matunzo?

 Ndiyo, siye Mashahidi wa Yehova tunakubali dawa na matunzo. Hata kama tunajikazaka kutunza miili yetu na kubakia na afya ya muzuri, wakati fulani tunakuwaka na “lazima ya munganga.” (Luka 5:31) Kusema kweli, sawa vile Luka, Mukristo wa karne ya kwanza, wamoja kati ya Mashahidi wa Yehova ni wanganga.​—Wakolosai 4:14.

 Hata vile, matunzo fulani inapingana na kanuni za Biblia; njo maana tunaikatalaka. Kwa mufano, tunakatalaka kutiwa damu mu mishipa juu Biblia inakataza kuitumia ili kuongeza nguvu mu mwili. (Matendo 15:20) Zaidi ya ile, Biblia inakataza matunzo ao namna ya matunzo yenye inatia ndani mambo ya uchawi.​—Wagalatia 5:19-21.

 Lakini, matunzo mingi haipingane na kanuni za Biblia. Kwa hiyo, kila mutu anajiamuliaka matunzo yenye anataka. Shahidi moya anaweza kuitika aina fulani ya dawa ao ya matunzo, lakini Shahidi mwingine anakatala aina ileile ya matunzo.​—Wagalatia 6:5.