Ona video zinazopatikana

BIBLIA INABADILISHA MAISHA

Nilipata Utajiri wa Kweli

Nilipata Utajiri wa Kweli
  • Alizaliwa: 1968

  • Inchi: Inchi ya Amerika

  • Historia: Mufanyabiashara mwenye alisali akuwe tajiri

MAISHA YANGU YA ZAMANI

 Nilikomalia mu familia ya Wakatoliki, katika Rochester, New York. Wazazi wangu walitengana wakati nilikuwa na miaka munane. Kwa hiyo, masiku ya katikati ya juma niliishi na mama yangu mu nyumba za watu maskini na miisho juma niliikala na baba yangu katika eneo ya matajiri. Wakati niliona vile mama yangu alikuwa anateseka juu ya kutukomalisha siye watoto wake sita, nilianza kuwaza tu vile napaswa kuwa tajiri juu ya kusaidia familia yangu.

 Baba yangu alitaka nikuwe na maisha ya muzuri, kwa hiyo alifanya mipango nitembelee masomo moja ya hali ya juu sana yenye ilikuwa inazoeza watu wakuwe wasimamizi wa ma hoteli. Niliipenda sana na mara moja nikajiandikisha na kuanza kusomea pale. Nilikuwa hakika kabisa kama Mungu amejibia sala yangu ya kuwa tajiri na mwenye furaha. Nilijifunza namna ya kusimamia hoteli, sheria ya biashara, na namna ya kutumikisha makuta za kompanyi kwa miaka tano. Wakati ileile nilifanya kazi katika hoteli yenye kazino mu muji wa Las Vegas, Nevada.

Kazi yangu ilitia ndani kuwapikia chakula matajiri wenye walicheza michezo ya makuta

 Wakati nilikuwa na miaka 22, nilikuwa vice-président wa hoteli yenye kazino. Nilionekana kuwa tajiri, mwenye maisha ya muzuri na mara mingi nilifurahia chakula ya muzuri sana na divai na pombe za bei kali. Marafiki wangu wenye tulifanya nao biashara walikuwa wananiambia: “Tafuta makuta bwana, kama hauna makuta mu hii dunia uko bure.” Waliona kama makuta njo inaleteaka mutu furaha ya kweli.

 Kazi yangu ilitia ndani kupikia chakula matajiri sana wenye walikuja ku Las Vegas ili kucheza michezo ya makuta. Hata kama walikuwa matajiri sana hawakukuwa na furaha. Na miye nilianza kukosa furaha. Kwa kweli, vile nilikuwa napata makuta ya mingi na njo vile mahangaiko iliongezeka na kukosa usingizi. Nilianza kuwaza nijiue. Sikupata furaha yenye nilikuwa nawazia kupata mu maisha, basi nikaanza kumuuliza Mungu, “Nitapata wapi furaha ya kweli?”

BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU

 Ile wakati, dada zangu wawili wenye walikuwa Mashahidi wa Yehova walihamia Las Vegas. Hata kama nilikatala vichapo vyao, niliitika kujifunza Biblia nao, nikitumia tu kopi yangu ya Biblia. Mu Biblia yangu, maneno yote ya Yesu ilikuwa imeandikwa na rangi ya mwekundu. Kwa kuwa nilikubali kila kitu kyenye Yesu alisema, dada zangu walitumia maneno ya Yesu juu ya kuzungumuza na miye. Tena, nilijisomea Biblia wakati nilikuwaka miye peke.

 Mambo mingi yenye nilisoma ilinishangaza. Kwa mufano, Yesu alisema: “Lakini wakati munasali, musiseme mambo yaleyale tena na tena, kama vile watu wa mataifa wanafanya, kwa maana wanafikiri watasikiwa kwa sababu wanatumia maneno mengi.” (Matayo 6:7) Lakini, padiri alinipatiaka picha ya Yesu na akaniambia kama nikisali kwa kutumia ile picha na kurudilia mara kumi sala ya Baba Yetu na mara kumi sala ya Maria Mutakatifu, Mungu atanipatia makuta ya mingi yenye nilikuwa nayo lazima. Lakini nilivumbula kama kufanya vile ilikuwa kusema mambo yaleyale tena na tena. Tena, nilisoma hii maneno ya Yesu: “Musimuite mutu yeyote baba yenu katika dunia, kwa maana Baba yenu ni mumoja, Ule wa mbinguni.” (Matayo 23:9) Basi, nikajiuliza tena, ‘Juu ya nini miye na Wakatoliki wenzangu tunaita mapadri wetu “Baba”?’

 Wakati nilifika mu kitabu ya Biblia ya Yakobo katika usomaji wangu, nilianza kufikiri sana juu ya maisha yangu. Katika sura ya 4, Yakobo ameandika hivi: “Hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi, kila atakaye kuwa rafiki wa dunia hujifanya kuwa adui wa Mungu.” (Yakobo 4:4, UV) Niliguswa zaidi na mustari wa 17: “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi.” Kisha niliita dada zangu kwenye telefone na kuwaambia kama naacha kazi yangu ya hoteli na kazino juu iliniingiza mu mambo yenye sikukubali, kutia ndani kucheza michezo ya makuta.

“Wakati nilifika mu kitabu ya Yakobo katika usomaji wangu, nilianza kufikiri zaidi juu ya maisha yangu”

 Nilipenda urafiki wangu na Mungu ukuwe muzuri, pia urafiki wangu na wazazi wangu, ndugu na dada zangu mu familia yetu. Basi nikaamua kutumia wakati wangu juu ya kufanya maisha yangu ikuwe mwepesi. Lakini haikukuwa mwepesi kufanya mabadiliko. Kwa mufano, nilipewa nafasi za kutumika na kupata makuta mingi mu mambo ya biashara ya kazino na hoteli. Waliniahidi hata kama nitapata mushahara mara mbili ao mara tatu kuliko ile yenye nilikuwaka nayo zamani. Lakini, kisha kusali juu ya ile jambo, niliamua kuachana kabisa na maisha ya vile. Niliacha kazi yangu, nikahamia katika garage yenye ilikuwa kwenye nyumba ya mama yangu na nikaanzisha biashara ndogo ya kuweka jalada menyu za mikahawa.

 Hata kama Biblia ilinisaidia kuwa na miradi yenye kufaa, nilikuwa bado siyaenda ku mikutano ya Mashahidi wa Yehova. Dada zangu waliniomba niwaambie kile kinanizuia. Niliwajibu hivi: “Mungu wenu Yehova, anatenganisha familia. Wakati pekee wenye ninaweza kuwa pamoja na familia ni katika sikukuu za Noeli na kuzaliwa, sikukuu zenye hamufanyake.” Dada yangu mumoja alianza kulia na iko ananiuliza: “Masiku ingine mu mwaka unakuwaka wapi? Siye tunapenda kuwa na weye kila siku. Lakini weye unapenda tu kuya wakati wa zile sikukuu juu tu inaomba ufanye vile.” Maneno yake ilinigusa, na miye nikaanza kulia naye.

 Wakati nilijua vile Mashahidi wa Yehova wanapendaka familia zao, tofauti kabisa na vile nilikuwa nawaza, niliamua kuenda ku mukutano moja ku Jumba la Ufalme. Wakati nilikuwa kule, nilikutana na Kevin, mwalimu wa Biblia mwenye uzoefu mwenye alianza kunifundisha Biblia.

 Kevin na bibi yake walikuwa na maisha ya mwepesi ili iwapatie nafasi ya kutumia wakati wao juu ya kusaidia watu wajue Biblia. Kiasi ya makuta yenye walipata iliwasaidia kutembelea Afrika na Amerika ya kati, ili kusaidia kujenga biro za tawi za Mashahidi. Walikuwa na furaha sana na walipendana sana. Nilijiambia, ‘Ningependa sana kuwa na maisha kama yao.’

 Kevin alinionyesha video yenye ilizungumuzia furaha ya kazi ya umisionere, na miye nikaamua kama ile njo kazi yenye napenda kufanya. Mu mwaka wa 1995, kisha kujifunza sana Biblia kwa miezi sita, nilibatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova. Kuliko kumuomba Mungu utajiri, nilisali na kusema: “Usinipatie umaskini wala utajiri.”​—Methali 30:8.

FAIDA YENYE NIMEPATA

 Sasa nimepata utajiri wa kweli hapana wa makuta, lakini wa kiroho. Nilikutana na bibi mupendwa Nuria, mu inchi ya Honduras. Na siye wote wawili tumetumikia mu Panama na Meksiko kama wamisionere. Hii maneno ya Biblia ni ya kweli kabisa: “Baraka ya Yehova ndiyo inamufanya mutu kuwa tajiri, Naye haongeze maumivu yoyote pamoja nayo”!​—Methali 10:22.