Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kusamehe huzima moto unaoweza kutokea mnapokosana

KWA WENZI WA NDOA

4: Kusameheana

4: Kusameheana

MAANA YAKE

Kusamehe kunamaanisha kuachilia kosa na kuondoa hisia zozote mbaya zinazotokana na jambo lililofanywa. Kusamehe hakumaanishi kupunguza uzito wa kosa au kujifanya kana kwamba halikutendeka.

KANUNI YA BIBLIA: “Endeleeni kuvumiliana na kusameheana kwa hiari hata ikiwa yeyote ana sababu ya kulalamika juu ya mwingine.” —Wakolosai 3:13.

“Unapompenda mtu, hukazii udhaifu wake, bali unaona sifa nzuri anazojitahidi kusitawisha.” —Aaron.

KWA NINI NI MUHIMU

Ukiweka kinyongo unaweza kuathiri afya yako ya mwili na ya kihisia, na pia unaweza kusababisha matatizo katika ndoa yenu.

“Siku moja, mume wangu aliniomba msamaha kwa sababu ya jambo alilofanya lililoniumiza sana. Haikuwa rahisi kwangu kumsamehe. Nilimsamehe baadaye, lakini nilijuta kwamba nilichelewa kufanya hivyo. Kutomsamehe haraka kulifanya uhusiano wetu uyumbe kiasi fulani.”—Julia.

MAMBO YA KUFANYA

JICHUNGUZE

Ikitokea tena kwamba mwenzi wako amesema au kufanya jambo linalokukasirisha, jiulize hivi:

  • ‘Je, ninakazia mambo madogo kupita kiasi?’

  • ‘Je, kosa alilofanya ni kubwa sana hivi kwamba anahitaji kuniomba msamaha, au ninaweza kuliachilia tu?’

ZUNGUMZA NA MWENZI WAKO

  • Kwa kawaida, sisi husameheana baada ya muda gani kupita?

  • Tunaweza kufanya nini ili tuwe tukisameheana bila kukawia?

MAPENDEKEZO

  • Unapokosewa, usikimbilie kufikiri kwamba mwenzi wako alikuwa na nia mbaya.

  • Jitahidi kufunika udhaifu wa mwenzi wako, ukikumbuka kwamba “sisi sote hujikwaa mara nyingi.”—Yakobo 3:2.

“Ni rahisi kusamehe unapohisi kwamba nyote mmekosea, lakini si rahisi ikiwa inaonekana mmoja ndiye aliyekosea. Unahitaji kuwa mnyenyekevu kutoka moyoni ili ukubali kumsamehe mtu.” —Kimberly.

KANUNI YA BIBLIA: “Suluhisha mambo upesi.”—Mathayo 5:25.

Ukiweka kinyongo unaweza kuathiri afya yako ya mwili na ya kihisia, na pia unaweza kusababisha matatizo katika ndoa yenu.