Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Tunaweza kupata furaha ya kweli kwa kushika sheria za Mungu

Watu Wanaomtii Mungu Wanapata Baraka

Watu Wanaomtii Mungu Wanapata Baraka

Nabii Musa alisema kwamba tukitii sheria za Mungu, tutapata baraka. (Kumbukumbu la Torati 10:13; 11:27) Hatumtii Mungu kwa sababu tunaogopa atatuadhibu. Sifa zake nzuri zinatuchochea kumtii kwa sababu tunampenda na hatutaki kumkasirisha. “Kumpenda Mungu humaanisha hivi, kwamba tuzishike amri zake.”​—1 Yohana 5:3.

Tunapata baraka gani tunapomtii Mungu? Fikiria baraka hizi mbili:

1. KUMTII MUNGU HUFANYA TUWE NA HEKIMA

“Mimi, Yehova, ni Mungu wako, ninayekufundisha ili ujifaidi mwenyewe, ninayekuongoza katika njia unayopaswa kutembea.”​—ISAYA 48:17.

Muumba wetu, Yehova Mungu, anatujua vizuri na anatuandalia mwongozo tunaohitaji. Ikiwa tunataka mafundisho ya Mungu yatusaidie kufanya maamuzi mazuri, tunapaswa kujifunza yale ambayo Mungu anataka tufanye, na kisha tuishi kulingana na mafundisho hayo.

2. KUMTII MUNGU HUFANYA TUWE NA FURAHA

“Wenye furaha ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika!”​—LUKA 11:28.

Leo, mamilioni ya watu wanaotii Neno la Mungu hupata furaha ya kweli. Kwa mfano, mwanamume fulani ambaye anaishi Hispania alikuwa mwenye hasira sana na aliwatendea wengine kikatili, kutia ndani mke wake. Siku moja, alisoma mambo ambayo nabii Musa aliandika kuhusu jinsi Yosefu, mwana wa Yakobo alivyokuwa mpole. Yosefu aliuzwa, akawa mtumwa na kufungwa isivyo haki. Hata hivyo, aliendelea kuwa mpole, mwenye kufanya amani na aliwasamehe wengine. (Mwanzo, sura ya 37-45) Mwanamume huyo alikiri hivi: “Kufikiria kuhusu mfano wa Yosefu kulinichochea kusitawisha upole, fadhili na kujizuia. Kwa sababu hiyo, sasa nina maisha yenye furaha.”

Maandiko Matakatifu yanatupatia miongozo ya jinsi tunavyopaswa kuwatendea wengine. Makala inayofuata itafafanua jambo hilo.