Kulingana na Luka 11:1-54

  • Jinsi ya kusali (1-13)

    • Sala ya mfano (2-4)

  • Roho waovu wafukuzwa kwa nguvu za Mungu (14-23)

  • Roho mwovu arudi (24-26)

  • Furaha ya kweli (27, 28)

  • Ishara ya Yona (29-32)

  • Taa ya mwili (33-36)

  • Ole kwa wanafiki wa kidini (37-54)

11  Sasa alikuwa mahali fulani akisali, alipomaliza, mmoja wa wanafunzi wake akamwambia: “Bwana, tufundishe jinsi ya kusali, kama vile Yohana alivyowafundisha wanafunzi wake.”  Basi akawaambia: “Mnaposali, semeni, ‘Baba, jina lako na litakaswe.*+ Ufalme wako na uje.+  Kila siku utupatie mkate wetu kulingana na mahitaji yetu.+  Na utusamehe dhambi zetu,+ kwa maana sisi pia humsamehe kila mtu aliye na deni letu;+ na usituingize katika majaribu.’”+  Kisha akawaambia: “Ikiwa mmoja wenu ana rafiki, naye aende kwake katikati ya usiku na kumwambia, ‘Rafiki, nikopeshe mikate mitatu,  kwa sababu rafiki yangu amekuja kwangu kutoka safarini nami sina kitu cha kumpa.’  Lakini yule aliye ndani amjibu: ‘Acha kunisumbua. Tayari mlango umefungwa, nami na watoto wangu tumelala. Siwezi kuamka nikupe chochote.’  Ninawaambia ingawa hataamka na kumpa chochote kwa sababu yeye ni rafiki yake, kwa hakika ataamka na kumpa kwa sababu anaendelea+ kumwomba.  Basi ninawaambia, endeleeni kuomba,+ nanyi mtapewa; endeleeni kutafuta, nanyi mtapata; endeleeni kupiga hodi, nanyi mtafunguliwa.+ 10  Kwa maana kila mtu anayeomba hupokea,+ na kila mtu anayetafuta hupata, na kila mtu anayepiga hodi atafunguliwa. 11  Kwa kweli, ni baba gani kati yenu ambaye mwana wake akiomba samaki, atampa nyoka?+ 12  Au pia akiomba yai, atampa nge? 13  Kwa hiyo, ingawa ninyi ni waovu, mnajua jinsi ya kuwapa watoto wenu zawadi nzuri, je, Baba aliye mbinguni hatawapa hata zaidi roho takatifu wale wanaomwomba!”+ 14  Baadaye alimfukuza roho mwovu aliye bubu.+ Roho huyo mwovu alipotoka, yule bubu akazungumza. Nao umati ukashangaa.+ 15  Lakini baadhi yao wakasema: “Anawafukuza roho waovu kwa nguvu za Beelzebuli,* mtawala wa roho waovu.”+ 16  Na wengine, ili kumjaribu, wakamwomba afanye ishara+ kutoka mbinguni. 17  Akijua mawazo yao,+ akawaambia: “Kila ufalme uliogawanyika dhidi yake wenyewe utaangamia, na nyumba iliyogawanyika dhidi yake yenyewe itaanguka. 18  Vivyo hivyo, ikiwa Shetani amegawanyika dhidi yake mwenyewe, ufalme wake utawezaje kusimama? Kwa maana mnasema ninafukuza roho waovu kupitia Beelzebuli. 19  Ikiwa ninawafukuza roho waovu kupitia Beelzebuli, wana wenu wanawafukuza kupitia nani? Hiyo ndiyo sababu watakuwa waamuzi wenu. 20  Lakini ikiwa ninawafukuza roho waovu kupitia kidole cha Mungu,+ kwa kweli Ufalme wa Mungu umewafikia ninyi ghafla.+ 21  Mtu mwenye nguvu aliye na silaha, anapolinda jumba lake, mali yake huwa salama. 22  Lakini mtu mwingine mwenye nguvu zaidi yake anapomshambulia na kumshinda, humnyang’anya silaha zake zote alizotegemea, naye hugawa vitu alivyompora. 23  Yeyote asiye upande wangu ananipinga, na yeyote asiyekusanya pamoja nami anatawanya.+ 24  “Roho mwovu anapomtoka mtu, yeye hupitia maeneo yasiyo na maji akitafuta mahali pa kupumzika, lakini anapokosa yeye husema, ‘Nitarudi kwenye nyumba yangu niliyoihama.’+ 25  Anapofika hukuta nyumba ikiwa imefagiwa ikawa safi na kupambwa. 26  Kisha huenda na kuwaleta roho wengine saba walio waovu kuliko yeye, na baada ya kuingia ndani, wao hukaa humo. Basi hali ya mwisho ya mtu huyo huwa mbaya zaidi kuliko ya kwanza.” 27  Alipokuwa akisema mambo hayo mwanamke fulani katika umati akasema kwa sauti kubwa: “Lenye furaha ni tumbo lililokubeba wewe na matiti uliyonyonya!”+ 28  Lakini Yesu akasema: “Hapana, badala yake, wenye furaha ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika!”+ 29  Umati ulipozidi kuongezeka, akaanza kusema: “Kizazi hiki ni kiovu; kinatafuta ishara, lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ishara ya Yona.+ 30  Kwa maana kama vile Yona+ alivyokuwa ishara kwa Waninawi, ndivyo Mwana wa binadamu atakavyokuwa kwa kizazi hiki. 31  Malkia wa kusini+ atasimamishwa katika hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki naye atakihukumu kwa sababu alikuja kutoka miisho ya dunia ili asikie hekima ya Sulemani. Lakini tazama! hapa pana mtu mkuu kuliko Sulemani.+ 32  Watu wa Ninawi watasimama katika hukumu pamoja na kizazi hiki nao watakihukumu, kwa sababu walitubu Yona alipowahubiria.+ Lakini tazama! hapa pana mtu mkuu kuliko Yona. 33  Hakuna mtu anayewasha taa na kuificha au kuiweka chini ya kikapu,* bali huiweka kwenye kinara cha taa,+ ili iwaangazie wale wanaoingia. 34  Taa ya mwili ni jicho lako. Ikiwa jicho lako linakazia jambo hususa,* mwili wako wote utakuwa mwangavu;* lakini ikiwa lina wivu,* mwili wako utakuwa na giza.+ 35  Basi, uwe mwangalifu ili nuru iliyo ndani yako isiwe ni giza. 36  Kwa hiyo, ikiwa mwili wako wote ni mwangavu bila giza lolote, utakuwa mwangavu kama taa inapokuangazia kwa mwanga wake.” 37  Baada ya kusema hayo, Farisayo mmoja alimwomba ale pamoja naye. Basi Yesu akaingia na kuketi mezani. 38  Hata hivyo, Farisayo huyo akashangaa kuona kwamba Yesu hakunawa* kabla ya kula.+ 39  Lakini Bwana akamwambia: “Ninyi Mafarisayo, husafisha upande wa nje wa kikombe na sahani, lakini ndani yenu mmejaa pupa na uovu.+ 40  Enyi wapumbavu! Yule aliyetengeneza nje ndiye aliyetengeneza ndani pia, sivyo? 41  Lakini toeni vitu vilivyo ndani viwe zawadi za rehema,* na tazama! mtakuwa safi katika mambo mengine yote. 42  Lakini ole wenu Mafarisayo, kwa sababu mnatoa sehemu ya kumi ya mnanaa na mchicha na kila aina ya mboga,+ lakini mnapuuza haki na kumpenda Mungu! Mlipaswa kufanya mambo hayo, bila kupuuza yale mengine.+ 43  Ole wenu Mafarisayo, kwa sababu mnapenda viti vya mbele* katika masinagogi na kusalimiwa sokoni!+ 44  Ole wenu, kwa sababu ninyi ni kama makaburi* yasiyoonekana,*+ ambayo watu hutembea juu yake bila kujua!” 45  Mtu fulani mwenye ujuzi wa Sheria akamwambia: “Mwalimu, unaposema mambo hayo, unatutukana sisi pia.” 46  Ndipo akasema: “Ole wenu pia ninyi mlio na ujuzi wa Sheria, kwa sababu mnawatwika watu mizigo mizito, lakini ninyi wenyewe hamwigusi hata kwa kidole kimoja!+ 47  “Ole wenu, kwa sababu mnajenga makaburi* ya manabii ambao mababu zenu waliwaua!+ 48  Hakika ninyi ni mashahidi wa matendo ya mababu zenu nanyi mnakubaliana nao, kwa sababu waliwaua manabii+ nanyi mnajenga makaburi yao. 49  Kwa sababu hiyo hekima ya Mungu ilisema: ‘Nitawatuma manabii na mitume kwao, lakini watawaua na kuwatesa baadhi yao, 50  ili damu ya manabii wote iliyomwagwa tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu idaiwe kutoka kwa kizazi hiki,+ 51  kuanzia damu ya Abeli+ mpaka damu ya Zekaria, aliyeuawa kati ya madhabahu na ile nyumba.’*+ Ndiyo, ninawaambia, kizazi hiki kitadaiwa* damu hiyo. 52  “Ole wenu ninyi wenye ujuzi wa Sheria, kwa sababu mliuondoa ufunguo wa ujuzi. Ninyi hamkuingia, na mnawazuia wale wanaoingia!”+ 53  Basi alipotoka hapo, waandishi na Mafarisayo wakaanza kumsonga sana na kumuuliza maswali mengi, 54  wakimtega ili wamnase kwa maneno yake.+

Maelezo ya Chini

Au “litukuzwe; lionwe kuwa takatifu.”
Jina lingine la Shetani.
Au “kikapu cha kupimia.”
Au “linaona vizuri.” Tnn., “ni rahisi.”
Au “utajawa na nuru.”
Tnn., “ni baya; lina uovu.”
Yaani, hakujisafisha kisherehe.
Au “ili kuwapa maskini zawadi.” Angalia Kamusi.
Au “vilivyo bora.”
Au “makaburi ya ukumbusho.”
Au “makaburi yasiyo na alama.”
Au “makaburi ya ukumbusho.”
Au “hekalu.”
Au “kitashtakiwa.”