Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Hadithi ya Pili ya Uwongo: Waovu Wanateseka Katika Moto wa Mateso

Hadithi ya Pili ya Uwongo: Waovu Wanateseka Katika Moto wa Mateso

Hadithi ya Pili ya Uwongo: Waovu Wanateseka Katika Moto wa Mateso

Ni nini chanzo cha hadithi hiyo? “Kati ya wanafalsafa wote Wagiriki wanaojulikana sana, yule aliyechochea sana mapokeo kuhusu Moto wa Mateso ni Plato.”—Histoire des enfers (Historia ya Moto wa Mateso), kilichoandikwa na Georges Minois, ukurasa wa 50.

“Kuanzia katikati ya karne ya 2 AD Wakristo ambao walijifunza kwa kadiri fulani falsafa za Kigiriki walianza kuona uhitaji wa kueleza imani yao kwa kutumia falsafa hizo . . . Falsafa ambayo iliwafaa zaidi ilikuwa ile ya Plato [mafundisho ya Plato].”—The New Encyclopædia Britannica (1988), Buku la 25, ukurasa wa 890.

“Mafundisho ya Kanisa yanathibitisha kwamba kuna moto wa mateso na ni wa milele. Mara tu baada ya kifo, nafsi za wale wanaokufa katika dhambi zinaenda kuzimu [moto wa mateso], mahali ambapo zinateswa kwa kuadhibiwa katika ‘moto wa milele.’ Adhabu kubwa ya kuzimu ni kutengwa milele na Mungu.”—Catechism of the Catholic Church (Katekisimu ya Kanisa Katoliki), chapa ya 1994, ukurasa wa 270.

Biblia inasema nini? “Maana walio hai wanajua ya kwamba watakufa: lakini wafu hawajui kitu, . . . maana hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima ndani ya kaburi [Sheol au kuzimu], pahali unapokwenda.”—Mhubiri 9:5, 10, Zaire Swahili Bible.

Neno la Kiebrania Sheol, ambalo linamaanisha “makao ya wafu,” linatafsiriwa kuwa “kuzimu” katika tafsiri fulani za Biblia. Andiko hilo linafunua nini kuhusu hali ya wafu? Je, wanateseka ndani ya Sheol ili walipie makosa yao? Hapana, kwa sababu “hawajui kitu.” Ndiyo sababu mzee wa ukoo Ayubu, alipokuwa akiteseka sana kwa sababu ya ugonjwa mbaya sana, alimwomba Mungu hivi: “Laiti ungenificha kuzimuni [Kiebrania, Sheol].” (Ayubu 14:13; Union Version) Ombi hilo lingekuwa na maana gani ikiwa Sheol au kuzimu ni mahali pa mateso ya milele? Katika Biblia, neno “kuzimu” linamaanisha tu kaburi, mahali ambapo hapana utendaji wowote.

Je, si kweli kwamba maelezo hayo kuhusu kuzimu yanapatana na akili na ni ya Kimaandiko? Hata hivyo, ni kosa gani baya zaidi ambalo linaweza kumfanya Mungu wa upendo amtese mtu milele? (1 Yohana 4:8) Lakini ikiwa moto wa mateso ni hadithi ya uwongo, namna gani kuhusu mbingu?

Linganisha mistari hii ya Biblia: Zaburi 146:3, 4; Matendo 2:25-27; Waroma 6:7, 23

UKWELI:

Mungu hawaadhibu watu katika moto wa mateso

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 5]

Barrators—Giampolo/The Doré Illustrations For Dante’s Divine Comedy/Dover Publications Inc.