Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Ni Nani Atakayeiokoa Dunia?

Ni Nani Atakayeiokoa Dunia?

 Watu wengi wanahangaishwa na jinsi wanadamu wameiharibu dunia na uhai uliomo. Kulingana na wataalamu fulani wa mazingira, wanyama fulani wanakabili hatari ya kutoweka na unamnanamna wa uhai duniani uko hatarini kuliko wakati mwingine kwa sababu ya matendo ya wanadamu.

 Je, wanadamu wataiangamiza dunia? Au je, watawahi kuishi kwa njia ambayo haiharibu mazingira?

Je, jitihada za wanadamu zitafanikiwa?

 Wataalamu wengi wana uhakika kwamba wanadamu wanaweza kuilinda dunia na kuishi kwa upatano na vitu vya asili. Watafiti fulani wamesema kwamba ili jitihada za wanadamu zifanikiwe, lazima mabadiliko yafanywe katika nyanja kadhaa kwa wakati uleule. Mabadiliko hayo yanatia ndani:

  •   Kuboresha jinsi ya kutunza ardhi, misitu, maeneo yenye maji mengi, na bahari.

  •   Kutumia njia tofauti za ukulima na kutafuta vyanzo vipya vya nishati.

  •   Kubadili jinsi chakula kinavyotokezwa na kusambazwa ili watu wale mazao ya mimea na kiasi kidogo tu cha nyama na samaki, na kwamba wanadamu wapunguze kiasi cha chakula wanachokula na wanachotupa.

  •   Kukubali kwamba ubora wa maisha hautegemei kuwa na vitu vingi vya kimwili.

 Una maoni gani? Je, inapatana na akili kutazamia serikali, biashara, na raia kushirikiana kwa njia kubwa hivyo? Au unafikiri kwamba inapatana na akili kutazamia kwamba pupa, ubinafsi, kutojali mambo ya wakati ujao kutazuia jitihada kama hizo?—2 Timotheo 3:1-5.

Sababu ya kuwa na tumaini

 Biblia inatuhakikishia kwamba wakati ujao wa sayari yetu hauko hatarini. Inatueleza kwa nini jitihada za wanadamu hazitoshi kuiokoa dunia, na inafafanua ni mabadiliko gani yanayohitajika. Pia inafafanua jinsi mabadiliko hayo yatakavyofanyika.

 Kwa nini jitihada za wanadamu pekee hazitoshi? Yehova a Mungu aliiumba dunia na aliwapa wanadamu jukumu la kuitunza. (Mwanzo 1:28; 2:15) Wangefanikiwa kutimiza mgawo huo ikiwa tu wangemtegemea Muumba wao ili kupata mwongozo na kutii maagizo yake. (Methali 20:24) Hata hivyo, walimkataa Yehova na kujaribu kujiamulia mambo. (Mhubiri 7:29) Bila msaada, wanadamu hawana uwezo wa kuitunza dunia, na jitihada zozote wanazofanya haziwezi kufanikiwa sana.—Methali 21:30; Yeremia 10:23.

 Badiliko ambalo lazima lifanyike. Mungu anakusudia kuwazuia wanadamu wasiiharibu dunia. (Ufunuo 11:18) Hataboresha serikali na jamii ya wanadamu wanaoiharibu sayari hii; badala yake, atawaondoa. (Ufunuo 21:1) Kwa sababu hiyo, Yehova anasema hivi: “Tazama! Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.”—Ufunuo 21:5.

 Jinsi badiliko hilo litakavyotokea. Yehova ataondoa serikali za wanadamu na kusimamisha serikali mbinguni inayoitwa Ufalme wa Mungu. Serikali hiyo, inayoongozwa na Yesu Kristo, itatawala juu ya dunia yote.—Danieli 2:44; Mathayo 6:10.

 Ufalme wa Mungu utawafundisha wanadamu jinsi ya kuishi kulingana na viwango vya Mungu vya uadilifu. Wanadamu watakapokubali kumsikiliza Muumba wao na kutii mwongozo wake, wataweza kuishi kwa upatano na vitu vya asili. (Isaya 11:9) Biblia inaonyesha jinsi serikali ya Mungu itakavyowawezesha raia wake kufurahia maisha bora, ambayo yatasaidia kuendeleza uhai duniani. Itafanya mambo yafuatayo:

 Unaweza kuwa na uhakika kwamba Ufalme wa Mungu utaleta mabadiliko hayo hivi karibuni. Ili kupata habari zaidi, ona makala yenye kichwa “Ufalme wa Mungu Utaanza Kutawala Dunia Lini?

a Yehova ndilo jina la kibinafsi la Mungu.—Zaburi 83:18.