Ufunuo kwa Yohana 11:1-19

  • Mashahidi wawili (1-13)

    • Watabiri kwa siku 1,260 wakiwa wamevaa nguo za magunia (3)

    • Wauawa na kuachwa bila kuzikwa (7-10)

    • Warudishwa kwenye uhai baada ya siku tatu na nusu (11, 12)

  • Ole wa pili umepita, wa tatu unakuja (14)

  • Tarumbeta ya saba (15-19)

    • Ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake (15)

    • Wale wanaoiharibu dunia wataharibiwa (18)

11  Nami nikapewa utete unaofanana na fimbo,*+ nikaambiwa: “Simama upime patakatifu pa hekalu la Mungu na madhabahu na wale wanaoabudu ndani yake.  Lakini kuhusu ua ulio nje ya patakatifu pa hekalu, uache wala usiupime, kwa sababu umepewa mataifa, nao watalikanyaga lile jiji takatifu+ chini ya miguu yao kwa miezi 42.+  Nitawafanya mashahidi wangu wawili watoe unabii kwa siku 1,260 wakiwa wamevaa nguo za magunia.”  Hao wanafananishwa na ile mizeituni+ miwili na vile vinara viwili vya taa,+ na wamesimama mbele za Bwana wa dunia.+  Yeyote akitaka kuwadhuru, moto hutoka katika vinywa vyao na kuwateketeza adui zao. Hivyo ndivyo anavyopaswa kuuawa mtu yeyote anayetaka kuwadhuru.  Hawa wana mamlaka ya kufunga anga*+ ili mvua isinyeshe+ katika siku zao za kutoa unabii, nao wana mamlaka juu ya maji ili kuyageuza kuwa damu+ na kuipiga dunia kwa kila aina ya mapigo mara nyingi wapendavyo.  Watakapomaliza kutoa ushahidi, yule mnyama wa mwituni anayepanda kutoka katika shimo refu lisilo na mwisho* atapigana nao na kuwashinda na kuwaua.+  Na maiti zao zitakuwa kwenye barabara kuu ya lile jiji kubwa ambalo katika maana ya kiroho linaitwa Sodoma na Misri, ambako pia Bwana wao aliuawa kwenye mti.  Na watu wa jamii na makabila na lugha na mataifa watazitazama maiti zao kwa siku tatu na nusu,+ wala hawataruhusu maiti zao zilazwe kaburini. 10  Na wale wanaokaa duniani wanashangilia juu yao na kusherehekea, nao watatumiana zawadi, kwa sababu hao manabii wawili waliwatesa watu wanaokaa duniani. 11  Baada ya zile siku tatu na nusu, roho ya uhai kutoka kwa Mungu ikaingia ndani yao,+ wakasimama kwa miguu yao, na woga mkubwa ukawaingia wale waliowaona. 12  Nao wakasikia sauti kubwa kutoka mbinguni ikiwaambia: “Pandeni mje huku.” Nao wakapanda kuingia mbinguni katika wingu, na adui zao wakawaona.* 13  Tetemeko kubwa la ardhi likatokea saa hiyo, na sehemu ya kumi ya jiji ikaanguka; na watu 7,000 wakauawa na tetemeko hilo la ardhi, na wale wengine wakawa na hofu na kumpa utukufu Mungu wa mbinguni. 14  Ole wa pili+ umepita. Tazama! Ole wa tatu unakuja upesi. 15  Malaika wa saba akaipiga tarumbeta yake.+ Na sauti kubwa zikasikika mbinguni, zikisema: “Ufalme wa ulimwengu umekuwa Ufalme wa Bwana wetu+ na wa Kristo wake,+ naye atatawala akiwa mfalme milele na milele.”+ 16  Na wale wazee 24+ waliokuwa wameketi kwenye viti vyao vya ufalme mbele za Mungu wakaanguka kifudifudi na kumwabudu Mungu, 17  wakisema: “Tunakushukuru wewe, Yehova* Mungu, Mweza-Yote, yule aliyeko+ na aliyekuwako, kwa sababu umechukua nguvu zako kuu na kuanza kutawala ukiwa mfalme.+ 18  Lakini mataifa wakawa na ghadhabu, nayo ghadhabu yako mwenyewe ikaja, na wakati uliowekwa ukafika kwa ajili ya kuhukumiwa kwa wafu na kuwapa thawabu+ watumwa wako manabii+ na watakatifu na wale wanaoliogopa jina lako, wadogo kwa wakubwa, na kuwaharibu wale wanaoiharibu dunia.”*+ 19  Na patakatifu pa hekalu la Mungu palipo mbinguni pakafunguliwa, na sanduku la agano lake likaonekana katika patakatifu pa hekalu lake.+ Na kukatokea radi na sauti na ngurumo na tetemeko la ardhi na mvua kubwa ya mawe.

Maelezo ya Chini

Au “fimbo ya kupimia.”
Au “mbingu.”
Au “abiso.” Angalia Kamusi.
Au “walikuwa wakiwatazama.”
Au “kuwaangamiza wale wanaoiangamiza dunia.”