Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 124

Washikamanifu Sikuzote

Washikamanifu Sikuzote

(Zaburi 18:25)

  1. 1. Tuwe washikamanifu,

    Kwake Yehova Mungu.

    Tuko wakfu kwake Yeye;

    Amri zake twatii.

    Sikuzote zatufaa,

    Twataka kuzijua.

    Tunaweza kumwamini.

    Kamwe hatutamwacha.

  2. 2. Tuwe washikamanifu,

    Kwa ndugu zetu wote.

    Na ikiwa wana shida,

    Hatutawasahau.

    Twawajali sikuzote,

    Kwa maneno na tendo.

    Ushirika wa kindugu,

    Unatuunganisha.

  3. 3. Tuwe washikamanifu,

    Kwa wanaoongoza.

    Tupatapo maagizo,

    Tutatii kikweli.

    Mungu atatubariki,

    Na kutuimarisha.

    Tutakuwa mali Yake,

    Tukiwa wa’minifu.