Zaburi 18:1-50

  • Kumsifu Mungu kwa sababu ya wokovu

    • “Yehova ni jabali langu” (2)

    • Yehova ni mshikamanifu kwa walio washikamanifu (25)

    • Njia ya Mungu ni kamilifu (30)

    • “Unyenyekevu wako hunifanya niwe mkuu” (35)

Kwa kiongozi. Wa Daudi mtumishi wa Yehova, aliyemwambia Yehova maneno ya wimbo huu siku ambayo Yehova alimwokoa kutoka mikononi mwa maadui wake wote na kutoka mikononi mwa Sauli. Alisema:+ 18  Ninakupenda, Ee Yehova, nguvu zangu.+   Yehova ni jabali langu na ngome yangu na Mwokozi wangu.+ Mungu wangu ni mwamba wangu,+ ninayemkimbilia,Ngao yangu na pembe* yangu ya wokovu,* kimbilio langu salama.*+   Ninamlilia Yehova, anayestahili kusifiwa,Nami nitaokolewa kutoka kwa maadui wangu.+   Kamba za kifo zilinizunguka;+Mafuriko ya ghafla ya watu wasiofaa kitu yaliniogopesha.+   Kamba za Kaburi* zilinizunguka;Mitego ya kifo ilinikabili.+   Katika taabu yangu nilimwita Yehova,Niliendelea kumlilia Mungu wangu anisaidie. Akiwa katika hekalu lake aliisikia sauti yangu,+Na kilio changu cha kumwomba msaada kilifika masikioni mwake.+   Kisha dunia ikaanza kutetemeka na kutikisika;+Misingi ya milima ikasukasukaNayo ikatikisika huku na huku kwa sababu alikuwa amekasirishwa.+   Moshi ulipanda kutoka katika mianzi ya pua yake,Na moto unaoteketeza kabisa ukatoka kinywani mwake;+Makaa ya mawe yanayowaka moto mkali yakatoka kwake.   Alizifanya mbingu zijikunje alipokuwa akishuka,+Na giza zito lilikuwa chini ya miguu yake.+ 10  Alipanda juu ya kerubi, akaja akiruka.+ Akashuka chini kwa ghafla juu ya mabawa ya kiumbe wa roho.*+ 11  Kisha akajifunika giza,+Pande zote kama banda,Maji yenye giza na mawingu mazito.+ 12  Kutoka katika mwangaza ulio mbele zakeMvua ya mawe na makaa ya mawe yanayowaka moto yakapasua mawingu. 13  Kisha Yehova akaanza kunguruma mbinguni;+Aliye Juu Zaidi aliifanya sauti yake isikike+Kwa mvua ya mawe na makaa ya mawe yanayowaka moto. 14  Alipiga mishale yake akawatawanya;+Alivurumisha radi yake akawavuruga.+ 15  Sakafu za vijito zikaonekana;*+Misingi ya nchi ikafunuliwa kwa kemeo lako, Ee Yehova,Kwa mlipuko wa pumzi kutoka katika mianzi ya pua yako.+ 16  Aliunyoosha mkono wake kutoka juu;Alinishika na kunivuta kutoka katika maji yenye kina.+ 17  Aliniokoa kutoka kwa adui yangu mwenye nguvu,+Kutoka kwa wale wanaonichukia, waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.+ 18  Walinikabili katika siku ya msiba wangu,+Lakini Yehova alikuwa tegemeo langu. 19  Alinitoa nje na kunileta mahali penye usalama;*Aliniokoa kwa sababu alipendezwa nami.+ 20  Yehova hunithawabisha kulingana na uadilifu wangu;+Hunilipa kulingana na usafi* wa mikono yangu.+ 21  Kwa maana nimezishika njia za Yehova,Nami sijamwacha kwa uovu Mungu wangu. 22  Hukumu zake zote ziko mbele yangu;Sitazipuuza sheria zake. 23  Nitabaki bila lawama mbele zake,+Nami nitajiepusha na uovu.+ 24  Yehova na anilipe kulingana na uadilifu wangu,+Kulingana na usafi* wa mikono yangu mbele zake.+ 25  Kwa mtu mshikamanifu unatenda kwa ushikamanifu;+Kwa mtu asiye na lawama unatenda bila lawama;+ 26  Kwa walio safi unajidhihirisha mwenyewe kuwa safi,+Lakini kwa waliopotoka unajidhihirisha mwenyewe kuwa mwenye busara.+ 27  Kwa maana wewe huwaokoa watu wa hali ya chini*+Lakini unawashusha wenye kiburi.*+ 28  Kwa maana ni wewe unayeiwasha taa yangu, Ee Yehova,Mungu wangu ambaye hulifanya giza langu liangaze.+ 29  Kwa msaada wako ninaweza kukabiliana na kundi la wavamizi;+Kwa nguvu za Mungu ninaweza kuupanda ukuta.+ 30  Njia ya Mungu wa kweli ni kamilifu;+Neno la Yehova ni safi.+ Yeye ni ngao kwa wote wanaomkimbilia.+ 31  Kwa maana ni nani aliye Mungu ila Yehova?+ Na ni nani aliye mwamba isipokuwa Mungu wetu?+ 32  Mungu wa kweli ndiye anayenivisha nguvu,+Naye ataifanya njia yangu iwe kamilifu.+ 33  Huifanya miguu yangu iwe kama ya paa;Hunifanya nisimame mahali palipo juu.+ 34  Huizoeza mikono yangu kupigana vita;Mikono yangu inaweza kuukunja upinde wa shaba. 35  Wewe hunipa ngao yako ya wokovu,+Mkono wako wa kuume hunitegemeza,*Na unyenyekevu wako hunifanya niwe mkuu.+ 36  Unapanua njia kwa ajili ya hatua zangu;Miguu yangu haitateleza.*+ 37  Nitawafuatia maadui wangu na kuwapita;Sitarudi mpaka watakapoangamizwa kabisa. 38  Nitawaponda wasiweze kuinuka;+Wataanguka chini ya miguu yangu. 39  Utanipa nguvu kwa ajili ya vita;Utawafanya maadui wangu waanguke chini yangu.+ 40  Utawafanya maadui wangu wanikimbie,*Nami nitawakomesha* wale wanaonichukia.+ 41  Wanalilia msaada, lakini hakuna mtu wa kuwaokoa;Hata wanamlilia Yehova, lakini yeye hawajibu. 42  Nitawaponda wawe laini kama mavumbi katika upepo;Nitawatupa nje kama matope barabarani. 43  Utaniokoa kutoka kwa watu wanaotafuta makosa.+ Utaniweka kuwa kiongozi wa mataifa.+ Watu ambao siwajui watanitumikia.+ 44  Watanitii watakaposikia fununu tu;Wageni watakuja wakijikunyata mbele zangu.+ 45  Wageni watakosa ujasiri;*Watakuja wakitetemeka kutoka katika ngome zao. 46  Yehova yuko hai! Mwamba wangu na asifiwe!+ Mungu wa wokovu wangu na akwezwe.+ 47  Mungu wa kweli hunilipizia kisasi;+Huyatiisha mataifa chini yangu. 48  Yeye huniokoa kutoka kwa maadui wangu wenye hasira;Unaniinua juu ya wale wanaonishambulia;+Unaniokoa kutoka kwa mtu mkatili. 49  Ndiyo sababu nitakutukuza wewe miongoni mwa mataifa, Ee Yehova,+Nami nitaliimbia sifa* jina lako.+ 50  Yeye hutenda matendo makuu ya wokovu kwa ajili ya mfalme wake;*+Humtendea mtiwa-mafuta wake kwa upendo mshikamanifu,+Kwa Daudi na kwa uzao wake* milele.+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “mwokozi wangu mwenye nguvu.”
Au “kilele changu salama.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “upepo.”
Au “Mifereji ya maji ikaonekana.”
Au “mahali penye nafasi kubwa.”
Au “ukosefu wa hatia.”
Au “ukosefu wa hatia.”
Au “wanaoteseka.”
Tnn., “unayashusha macho ya kiburi.”
Au “hunidumisha.”
Au “Vifundo vya miguu yangu havitateleza.”
Au “Utanionyesha migongo ya maadui wangu.”
Au “nitawanyamazisha.”
Au “watafifia.”
Au “nitalipigia muziki.”
Au “humpa ushindi mkubwa mfalme wake.”
Tnn., “mbegu yake.”