Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Kifaa hiki cha kujifunzia Biblia kimekusudiwa kukusaidia kujifunza yale ambayo Biblia inasema kuhusu masomo tofauti-tofauti, kutia ndani kwa nini tunateseka, ni nini hutupata tunapokufa, tunawezaje kuwa na maisha ya familia yenye furaha, na mengine mengi.

Je, Hivi Ndivyo Mungu Alivyokusudia?

Huenda ukashangaa kwa nini kuna matatizo mengi leo. Je, unajua kwamba Biblia inaeleza kuhusu mabadiliko halisi yajayo ambayo unaweza kufaidika kutokana nayo?

SURA YA 1

Ukweli Kumhusu Mungu

Je, unafikiri Mungu anakujali wewe kibinafsi? Jifunze kuhusu utu wake na jinsi ambavyo unaweza kumkaribia.

SURA YA 2

Biblia—Kitabu Kutoka kwa Mungu

Biblia inaweza kukusaidiaje kukabili matatizo yako binafsi? Kwa nini unaweza kuutumaini unabii wake?

SURA YA 3

Mungu Ana Kusudi Gani kwa Dunia?

Je, kusudi la Mungu kwa dunia kuwa paradiso litafanikiwa? Ikiwa ndiyo, ni lini?

SURA YA 4

Yesu Kristo Ni Nani?

Jifunze kwa nini Yesu ni Masihi aliyeahidiwa, Yesu alitoka wapi, kwa nini ni mwana mzaliwa pekee wa Yehova.

SURA YA 5

Fidia—Zawadi Bora Zaidi Kutoka kwa Mungu

Fidia ni nini? Unaweza kufaidikaje kutokana nayo?

SURA YA 6

Wafu Wako Wapi?

Jifunze yale ambayo Biblia inasema kuhusu mahali ambapo wafu wako na kwa nini wanadamu hufa.

SURA YA 7

Tumaini Hakika kwa Wapendwa Wako Ambao Wamekufa

Je, umempoteza mpendwa wako katika kifo? Je, inawezekana kuwaona tena? Jifunze yale ambayo Biblia inasema kuhusu kifo.

SURA YA 8

Ufalme wa Mungu Ni Nini?

Watu wengi wanaijua sala ya Bwana. Maneno “ufalme wako na uje” yanamaanisha nini?

SURA YA 9

Je, Tunaishi Katika “Siku za Mwisho”?

Jifunze jinsi matendo na mtazamo wa watu wanaotuzunguka unavyoonyesha kwamba sasa tunaishi katika “siku za mwisho” ambazo Biblia ilitabiri.

SURA YA 10

Jinsi Viumbe wa Roho Wanavyohusika Maishani Mwetu

Biblia inazungumzia kuhusu malaika na roho waovu. Je, viumbe hao wa roho wanaweza kuwa halisi? Je, wanaweza kukuathiri?

SURA YA 11

Kwa Nini Mungu Anawaacha Watu Wateseke?

Watu wengi wanafikiri kwamba Mungu ndiye wa kulaumiwa kwa sababu ya mateso yote yanayotokea ulimwenguni. Je, wewe una maoni gani? Jifunze yale ambayo Mungu anasema kuhusu sababu za watu kuteseka.

SURA YA 12

Kuishi Maisha Yanayompendeza Mungu

Je, inawezekana kuishi maisha yanayompendeza Mungu? Kwa kweli, unaweza kuwa rafiki yake.

SURA YA 13

Maoni ya Mungu Kuhusu Uhai

Mungu anaonaje kutoa mimba, kutia damu mishipani, na uhai wa wanyama?

SURA YA 14

Jinsi ya Kufanya Maisha ya Familia Yako Yawe Yenye Furaha

Upendo wa Yesu ni mfano mzuri ambao waume, wake, wazazi, na watoto wanaweza kuiga. Tunajifunza nini kutoka kwake?

SURA YA 15

Ibada Ambayo Mungu Anakubali

Chunguza mambo sita ambayo yanawatambulisha wafuasi wa dini ya kweli.

SURA YA 16

Chukua Msimamo Upande wa Ibada ya Kweli

Unaweza kukabiliana na hali gani unapowaeleza wengine kuhusu imani yako? Unawezaje kuzungumza nao bila kuwakasirisha?

SURA YA 17

Mkaribie Mungu Katika Sala

Je Mungu anakusikiliza unaposali? Ili ujibu swali hilo, unahitaji kuelewa kile ambacho Biblia inafundisha kuhusu sala.

SURA YA 18

Ubatizo na Uhusiano Wako Pamoja na Mungu

Mtu anapaswa kuchukua hatua gani ili astahili kubatizwa? Jifunze kinachomaanishwa na ubatizo na jinsi unavyopaswa kufanywa.

SURA YA 19

Kaa Katika Upendo wa Mungu

Tunawezaje kuonyesha shukrani kwa ajili ya yote ambayo Mungu ametufanyia?

NYONGEZA

Jina la Mungu—Maana na Matumizi

Jina la Mungu limeondolewa katika tafsiri nyingi za Biblia. Kwa nini? Je, ni muhimu kutumia jina la Mungu?

NYONGEZA

Jinsi Unabii wa Danieli Ulivyotabiri Kutokea kwa Masihi

Zaidi ya miaka 500 mapema, Mungu alifunua wakati hususa ambao Masihi angetokea. Jifunze kuhusu unabii huo wenye kusisimua!

NYONGEZA

Yesu Kristo—Masihi Aliyeahidiwa

Yesu alitimiza unabii wote wa Biblia kuhusu Masihi. Chunguza katika Biblia yako uone jinsi unabii huo ulivyotimizwa kikamili.

NYONGEZA

Ukweli Kuhusu Baba, Mwana, na Roho Takatifu

Watu wengi wanaamini kwamba fundisho la Utatu linaungwa mkono na Biblia. Je, ni kweli?

NYONGEZA

Kwa Nini Wakristo wa Kweli Hawatumii Msalaba Katika Ibada?

Je, kweli Yesu alikufa juu ya msalaba? Pata jibu kutoka kwenye Biblia.

NYONGEZA

Mlo wa Jioni wa Bwana—Maadhimisho Yanayomletea Mungu Heshima

Wakristo wanaamriwa waadhimishe Ukumbusho wa kifo cha Kristo, maadhimisho hayo yanaitwa pia Mlo wa Jioni wa Bwana. Yanapaswa kufanywa wakati gani na jinsi gani?

NYONGEZA

Maneno “Nafsi” na “Roho” Yanamaanisha Nini Hasa?

Watu wengi wanafikiri kwamba mtu anapokufa kitu fulani hutoka ndani ya mwili wa mwanadamu na kuendelea kuishi. Neno la Mungu linatufundisha nini kuhusu hilo?

NYONGEZA

Sheoli na Hadesi Zinamaanisha Nini?

Tafsiri fulani za Biblia hutumia maneno “kaburi” au “kuzimu” kumaanisha Sheoli na Hadesi. Maneno hayo yanamaanisha nini hasa?

NYONGEZA

Siku ya Hukumu Ni Nini?

Soma uone jinsi wanadamu wote waaminifu watakavyobarikiwa katika Siku ya Hukumu.

NYONGEZA

1914—Mwaka Muhimu Katika Unabii wa Biblia

Kuna uthibitisho gani wa Kimaandiko unaoonyesha kwamba 1914 ulikuwa mwaka muhimu?

NYONGEZA

Yule Malaika Mkuu Mikaeli Ni Nani?

Biblia inamtambulisha malaika huyo mkuu na mwenye nguvu. Soma zaidi kumhusu na yale anayofanya sasa.

NYONGEZA

Kumtambulisha “Babiloni Mkubwa”

Kitabu cha Ufunuo kinamzungumzia mwanamke anayeitwa “Babiloni Mkubwa.” Je, ni mwanamke halisi? Biblia inatueleza nini kuhusu mwanamke huyo?

NYONGEZA

Je, Yesu Alizaliwa Desemba?

Fikiria hali ya hewa katika mwezi ambao Yesu alizaliwa. Tunapata somo gani?

NYONGEZA

Je, Tusherehekee Sikukuu?

Sikukuu zinazopendwa na watu wengi katika eneo unaloishi zilianzaje? Huenda jibu la swali hilo likakustaajabisha.