Hamia kwenye habari

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova Ni Nini?

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova Ni Nini?

 Baraza Linaloongoza ni kikundi kidogo cha Wakristo wakomavu wanaoongoza kazi ya Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote. Kazi yao inahusisha mambo mawili:

 Baraza Linaloongoza hufuata kielelezo kilichowekwa katika karne ya kwanza na “mitume na wanaume wazee katika Yerusalemu,” ambao walifanya maamuzi muhimu kwa ajili ya kutaniko lote la Kikristo. (Matendo 15:2) Kama tu wanaume hao waaminifu, washiriki wa Baraza Linaloongoza si viongozi wa tengenezo letu. Wanaitegemea Biblia ili kupata mwongozo, na wanakubali kwamba Yehova Mungu amemweka Yesu Kristo rasmi kuwa Kichwa cha kutaniko.​—1 Wakorintho 11:3; Waefeso 5:23.

Washiriki wa Baraza Linaloongoza ni akina nani?

 Washiriki wa Baraza Linaloongoza ni Kenneth Cook, Jr., Samuel Herd, Geoffrey Jackson, Stephen Lett, Gerrit Lösch, Anthony Morris III, Mark Sanderson, na David Splane. Wanatumikia katika makao yetu makuu yaliyoko Warwick, New York, Marekani.

Baraza Linaloongoza limepangwa jinsi gani?

 Baraza Linaloongoza lina halmashauri sita zinazosimamia sehemu mbalimbali za kazi yetu, na kila mshiriki wa baraza hilo anatumikia katika halmashauri moja au zaidi.

  •   Halmashauri ya Waratibu: Inasimamia mambo ya kisheria na kushughulikia utoaji wa msaada wakati wa misiba, au mmoja wa waamini wenzetu anapoteswa kwa sababu ya imani ya kidini, au jambo lingine la dharura linalowahusu Mashahidi wa Yehova linapotokea.

  •   Halmashauri ya Wafanyakazi: Inasimamia mipango inayowahusu washiriki wa familia ya Betheli.

  •   Halmashauri ya Utangazaji: Inasimamia uchapishaji na usafirishaji wa machapisho ya Biblia na ujenzi wa mahali pa mikutano, ofisi za utafsiri, na ofisi za tawi.

  •   Halmashauri ya Utumishi: Inasimamia kazi ya kuhubiri “habari njema ya ufalme.”​—Mathayo 24:14.

  •   Halmashauri ya Ufundishaji: Inaongoza kutayarishwa kwa elimu ya kiroho inayotolewa kupitia mikutano, shule, na rekodi za sauti na video.

  •   Halmashauri ya Uandikaji: Inaongoza kutayarishwa kwa elimu ya kiroho iliyochapishwa na iliyo kwenye tovuti yetu na inasimamia kazi ya kutafsiri.

 Mbali na kazi inayofanywa kupitia kwa halmashauri hizi, Baraza Linaloongoza linakutana kila juma ili kufikiria kuhusu mahitaji ya tengenezo letu. Katika mikutano hiyo, washiriki hao huzungumzia mambo yanayotajwa katika Maandiko, na wanajitiisha kwa roho takatifu ya Mungu, wakijitahidi kufikia maamuzi ya pamoja.​—Matendo 15:25.

Wasaidizi wa Baraza Linaloongoza ni akina nani?

 Ni Wakristo wanaoaminika ambao husaidia katika halmashauri za Baraza Linaloongoza. (1 Wakorintho 4:2) Wana uwezo na uzoefu wa kufanya kazi inayosimamiwa na halmashauri waliyogawiwa, na wanahudhuria mikutano ya kila juma inayofanywa na halmashauri hiyo. Ingawa hawashiriki katika kufanya maamuzi, wasaidizi hao hutoa mashauri yenye thamani na habari za ziada, wanahakikisha maamuzi ya halmashauri hiyo yametimizwa, na wanakagua jinsi maamuzi hayo yanavyotekelezwa. Pia wanaweza kupewa mgawo na Baraza Linaloongoza kutembelea ndugu zetu katika sehemu mbalimbali ulimwenguni au kutoa hotuba katika matukio kama vile mkutano wa kila mwaka na kuhitimu kwa shule ya Gileadi.

ORODHA YA WASAIDIZI

Halmashauri

Jina

Waratibu

  • Ekrann, John

  • Gillies, Paul

Wafanyakazi

  • Grizzle, Gerald

  • LaFranca, Patrick

  • Molchan, Daniel

  • Walls, Ralph

  • Winder, Jeffrey

Utangazaji

  • Butler, Robert

  • Corkern, Harold

  • Glockentin, Gajus

  • Gordon, Donald

  • Luccioni, Robert

  • Reinmueller, Alex

  • Sinclair, David

Utumishi

  • Breaux, Gary

  • Dellinger, Joel

  • Fleegle, Gage

  • Hyatt, Seth

  • Mavor, Christopher

  • Perla, Baltasar, Jr.

  • Smith, Jonathan

  • Turner, William, Jr.

  • Weaver, Leon, Jr.

Ufundishaji

  •  Curzan, Ronald

  • Flodin, Kenneth

  • Malenfant, William

  • Noumair, Mark

  • Schafer, David

Uandikaji

  • Ciranko, Robert

  • Mantz, James

  • Marais, Izak

  • Myers, Leonard

  • Smalley, Gene

  • van Selm, Hermanus