Hamia kwenye habari

Je, Mashahidi wa Yehova Hukubali Matibabu?

Je, Mashahidi wa Yehova Hukubali Matibabu?

 Ndiyo, Mashahidi wa Yehova hukubali dawa na matibabu. Ingawa tunajitahidi kutunza miili yetu na kudumisha afya nzuri, nyakati nyingine ‘tunamhitaji daktari.’ (Luka 5:31, Biblia Habari Njema) Kwa kweli, sawa tu na Luka, Mkristo wa karne ya kwanza, baadhi ya Mashahidi wa Yehova ni madaktari.—Wakolosai 4:14.

 Hata hivyo, matibabu fulani yanapingana na kanuni za Biblia, na tunakataa matibabu hayo. Kwa mfano, hatukubali kutiwa damu mishipani kwa sababu Biblia inakataza kutumia damu kuutibu mwili. (Mdo. 15:20) Biblia pia inakataza matibabu yanayotia ndani mazoea ya kichawi.—Wagalatia 5:19-21.

 Hata hivyo, matibabu mengi hayapingani na kanuni za Biblia. Kwa hiyo, kila mtu hujiamulia mwenyewe matibabu anayotaka. Shahidi mmoja anaweza kukubali aina fulani ya dawa au matibabu, na mwingine anaweza kukataa matibabu hayo.—Wagalatia 6:5.