Ona video zinazopatikana

Mungu Anapenda Ufanye Nini?

Mungu Anapenda Ufanye Nini?

Jibu la Biblia

 Mungu anataka umujue vizuri zaidi, uwe rafiki yake na umupende na kumutumikia kwa moyo wako wote. (Mathayo 22:37, 38; Yakobo 4:8) Unaweza kujua yale ambayo Mungu anapenda ufanye kwa kuchunguza maisha na mafundisho ya Yesu. (Yohana 7:16, 17) Yesu hakuzungumuzia tu mapenzi ya Mungu—aliyafanya. Kwa hiyo, Yesu alisema kwamba kusudi lake katika maisha lilikuwa ‘kufanya, si mapenzi yake, bali mapenzi yake aliyemutuma.’—Yohana 6:38.

Je, ninahitaji ishara, maono, ao mwito wa pekee ili kujua yale ambayo Mungu anapenda nifanye?

 Hapana, kwa sababu Biblia ina ujumbe wa Mungu kwa wanadamu. Biblia inakutolea kila kitu unachohitaji ile uwe na “vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.” (2 Timotheo 3:16, 17) Mungu anataka utumie Biblia pamoja na “nguvu ya kufikiri” ili kujua yale ambayo anapenda ufanye.—Waroma 12:1, 2; Waefeso 5:17.

Je, ninaweza kabisa kufanya mapenzi ya Mungu?

 Ndiyo kabisa, unaweza, kwa sababu Biblia inasema hivi: “Amri zake [za Mungu] si ngumu.” (1 Yohana 5:3, Biblia Habari Njema) Hilo halimaanishe kwamba ni rahisi siku zote kutii amri za Mungu. Lakini faida utakazopata ni nyingi sana kuliko jitihada unazoweza kufanya. Yesu mwenyewe alisema hivi: “Heri zaidi wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika!”—Luka 11:28, Biblia Habari Njema.