Ona video zinazopatikana

Ufalme wa Mungu Uko mu Moyo Wako?

Ufalme wa Mungu Uko mu Moyo Wako?

Jibu ya Biblia

 Hapana, Ufalme wa Mungu hauko mu moyo wa Wakristo. * Biblia inaonyesha kwenye Ufalme wa Mungu uko wakati inauita kuwa “ufalme wa mbinguni.” (Matayo 4:17, La Sainte Bible en swahili de la R.D.Congo) Ona namna Biblia inaonyesha kama Ufalme wa Mungu ni serikali ao guvernema yenye iko natawala ikiwa mbinguni.

 Biblia haifundishe kama Ufalme wa Mungu unatawala ndani ya moyo wa mutu. Lakini, inafundisha kama “neno la Ufalme” ao “habari njema ya Ufalme” inaweza kugusa mioyo yetu na inapaswa kufanya vile.​—Matayo 13:19; 24:14.

Maneno “ufalme wa Mungu umo ndani yenu,” maana yake nini?

 Watu fulani wanashindwa kuelewa fasi kwenye Ufalme wa Mungu uko juu ya namna tafsiri fulani za Biblia zinatafsiri Luka 17:21. Kwa mufano, tafsiri Union Version inatafsiri ile andiko hivi: “Ufalme wa Mungu umo ndani yenu.” Juu tuelewe muzuri ile andiko, tunapaswa kufikiria ni watu gani Yesu aliambia ile maneno.

Ufalme wa Mungu haukukuwa ndani ya mioyo ya watu wabaya na wenye walikuwa napenda kumuua Yesu

 Yesu alikuwa nazungumuza na Wafarisayo, viongozi wa dini wenye walikuwa namupinga na wenye walikuwa natafuta kumuua. (Matayo 12:14; Luka 17:20) Unawaza kabisa Ufalme wa Mungu ulikuwa mu mioyo ya wale watu wabaya? Yesu aliwaambia hivi: “Mumejaa unafiki na uvunjaji wa sheria.”​—Matayo 23:27, 28.

 Tafsiri zingine zinatafsiri muzuri maneno ya Yesu mu Luka 17:21: “Ufalme wa Mungu uko kati yenu.” (Italiki ni zetu; Habari Njema) “Ufalme wa Mungu uko katikati yenu.” (Tafsiri ya Ulimwengu Mupya) Ufalme wa Mungu ulikuwa “kati” ao “katikati ya” Wafarisayo, juu Yesu, mwenye angekuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu alikuwa katikati yao.​—Luka 1:32, 33.

^ Dini za mingi za Kikristo zinafundishaka kama Ufalme wa Mungu uko mu moyo wa mutu. Kwa mufano, mu Amerika, Kanisa ya Kibatisti ya Kusini ilisema kama Ufalme wa Mungu ni sehemu ya “utawala wa Mungu mu moyo na mu maisha ya mutu.” Vilevile, mu kitabu Jesus of Nazareth, Papa Benedikto wa 16, alisema kama “Ufalme wa Mungu unakuya wakati tuko na moyo mutiifu.”