Zaburi 110:1-7

  • Mufalme na kuhani kama Melkisedeki

    • ‘Tawala katikati ya maadui wako’ (2)

    • Vijana wenye wanajitoa kwa kujipendea ni kama matone ya umande (3)

Ya Daudi. Muziki. 110  Yehova alimuambia Bwana wangu: “Kaa kwenye mukono wangu wa kuume+ Mupaka niweke maadui wako kuwa kiti cha miguu yako.”+   Yehova atanyoosha fimbo ya ufalme ya nguvu zako kutoka Sayuni, na kusema: “Uende utawale katikati ya maadui wako.”+   Watu wako watajitoa kwa kujipendea katika siku ya jeshi lako.* Katika utakatifu wenye kupendeza sana, kutoka katika tumbo la uzazi la mapambazuko,* Uko na kikundi chako cha vijana kama vile matone ya umande.   Yehova ameapa kiapo na hatabadilisha mawazo yake:* “Wewe ni kuhani milele+ Kwa mufano wa Melkisedeki!”+   Yehova atakuwa kwenye mukono wako wa kuume;+ Ataponda wafalme katika siku ya kasirani yake.+   Ataleta hukumu juu ya* mataifa;+ Atajaza maiti katika inchi.+ Ataponda kiongozi wa* inchi kubwa sana.*   Yeye* atakunywa maji ya muto mudogo wenye kuwa pembeni ya barabara. Kwa hiyo, atainua juu kichwa chake.

Maelezo ya Chini

Ao “siku yenye jeshi lako litajitayarisha kwa ajili ya vita.”
Mapambazuko ni wakati mwangaza wa asubui unaanza kutokea.
Ao “hatasikitika.”
Ao “kati ya.”
Tnn., “kichwa cha.”
Ao “dunia yote.”
Mwenye kuzungumuziwa ni “Bwana wangu” ambaye anatajwa katika mustari wa 1.