Ona video zinazopatikana

VIJANA WANAULIZA

Biblia Inaweza Kunisaidia Namna Gani?​—Sehemu ya 1: Ujue Muzuri Biblia Yako

Biblia Inaweza Kunisaidia Namna Gani?​—Sehemu ya 1: Ujue Muzuri Biblia Yako

 “Nimepima kusoma Biblia, lakini ninavunjikaka moyo juu ni kitabu ya kabambi sana!”​—Briana, 15.

 Na weye unajisikiaka vile? Hii habari itakusaidia!

 Juu ya nini ni muzuri usome Biblia?

 Unaonaka kusoma Biblia kuwa jambo ya kuchokesha sana? Kama ni vile, hauko weye peke. Unaweza kuona Biblia kuwa kitabu ya kabambi yenye iko na kurasa zaidi ya elfu moja na maandishi ya kidogo-kidogo na haina picha. Unaweza kuona kama kuliko kusoma Biblia, afazali uangalie televizyo ao video!

 Lakini, pima kuwaza hivi: Kama unapata sanduku ya kuwekea vitu vya maana sana, hautapenda kujua nini njo iko ndani?

 Biblia nayo iko sawa vile ile sanduku. Ndani yake muko mashauri ya mingi ya muzuri yenye inaweza kukusaidia

  •   Kukamata maamuzi ya muzuri

  •   Kusikilizana na wazazi wako

  •   Kupata marafiki wazuri

  •   Kujua mambo ya kufanya wakati uko na mahangaiko

 Juu ya nini ile kitabu ya zamani iko na faida sana leo? Ni juu “kila andiko liliongozwa na roho ya Mungu.” (2 Timoteo 3:16) Ni kusema, mashauri yenye iko mu Biblia inatoka kwa mutu mwenye iko hekima zaidi.

Biblia iko sawa vile sanduku yenye ndani yake muko mashauri mingi yenye hekima

 Unapaswa kusoma Biblia namna gani?

 Njia moja ni kusoma Biblia kuanzia mwanzo mupaka mwisho. Kufanya vile kutakusaidia ujue wazo kubwa yenye Biblia inazungumuzia. Kuko njia za mingi za kusoma Biblia. Tuone mifano mbili:

  •    Unaweza kusoma vitabu 66 vya Biblia kwa kufuata namna vinapangwa, kuanzia Mwanzo mupaka Ufunuo.

  •    Unaweza kusoma Biblia kulingana na vile matukio ilifuatana.

 Shauri: Nyongeza A7 mu Tafsiri ya Ulimwengu Mupya inaonyesha namna matukio makubwa mu maisha ya Yesu hapa ku dunia ilifuatana.

 Njia ya pili ya kusoma Biblia ni kuchagula habari yenye inazungumuzia tatizo fulani yenye uko nayo. Kwa mufano:

  •   Unapenda kupata marafiki wenye kutumainika? Soma habari ya Yonatani na Daudi. (1 Samweli, sura 18-​20) Tafuta kujua ni sifa gani zenye Daudi alikuwaka nazo zenye zilifanyaka Yonatani amupende.

  •   Unapenda kujua namna ya kupinga majaribu? Soma habari ya Yosefu na uone namna alishindaka jaribu. (Mwanzo, sura ya 39) Tafuta kujua nani njo alipatiaka Yosefu nguvu ya kushinda jaribu.

  •   Ungependa kujua namna sala inaweza kukusaidia? Soma habari ya Nehemia. (Nehemia, sura ya 2) Tafuta mambo yenye inaonyesha kama Mungu alijibiaka sala ya Nehamia.

 Shauri: Wakati uko nasoma Biblia, tafuta fasi ya kimya, juu akili yako ikale fasi moya.

 Nji ya tatu ya kusoma Biblia ni kuchagula habari ao zaburi fulani, kuisoma, na kisha kuona namna unaweza kuitumikisha. Kisha kusoma, ujiulize maulizo sawa hii:

  •    Juu ya nini Yehova aliandikishaka hii habari?

  •    Inanifundisha nini juu ya sifa za Yehova ao namna yake ya kufanya mambo?

  •    Namna gani ninaweza kutumikisha hii habari mu maisha yangu?

 Shauri: Upange kusoma Biblia. Andika siku yenye unapenda kuanza kusoma Biblia kwa kutumia Programu ya Usomaji wa Biblia yenye iko ku jw.org.