Ona video zinazopatikana

VIJANA WANAULIZA

Namna Gani Ninaweza Kuepuka Mawazo ya Mubaya?

Namna Gani Ninaweza Kuepuka Mawazo ya Mubaya?

 Unajionaka namna gani?

  •   Niko na mutazamo muzuri

     “Ninajikaza kuwa mwenye furaha na mwenye kuepuka kukasirika. Ninapenda kuwa na sura yenye furaha kila siku.”—Valerie.

  •   Niko na mutazamo mubaya

     “Wakati jambo la muzuri linatokea, mara moja ninawaza kama haiwezi kuwa kweli, ao haiwezekane.”—Rebecca.

  •   Niko na mawazo yenye kufaa

     “Kama niko na mutazamo muzuri nitavunjika moyo wakati mambo haiende muzuri, na kama niko na mutazamo mubaya nitaishi bila furaha. Kuwa na mawazo yenye kufaa kunanisaidia nione mambo vile iko kwa kweli.”—Anna.

 Juu ya nini ni jambo la maana?

 Biblia inasema kama “mutu mwenye moyo wa furaha iko na karamu sikuzote.” (Mezali 15:15) Ni wazi kuwa, mara mingi watu wenye kuepuka mawazo ya mubaya na wenye kuwa na mawazo ya muzuri juu ya maisha, wanakuwaka na furaha. Wanaweza pia kuwa na marafiki wengi. Kusema kweli, ni nani anapendaka kupitisha wakati na watu wenye kuwa na huzuni kila mara?

 Lakini, hata kama uko mutu mwenye kuwa na mutazamo muzuri unaweza tu kupata magumu. Kwa mufano:

  •   Kila mara vyombo vya habari vinatangaza mambo ya vita, ugaidi (terrorisme), ao matendo ya kuvunja sheria.

  •   Unaweza kupambana na matatizo katika familia yako.

  •   Bila shaka uko unapambana na uzaifu wako mwenyewe.

  •   Rafiki yako anaweza kukuhuzunisha.

 Kuliko kufanya kama vile ile matatizo haiko, ao kuikazia akili sana, ujikaze kuwa na mawazo yenye kufaa juu ya ile matatizo. Kuwa na mawazo yenye kufaa kutakusaidia usikuwe na mawazo ya mubaya kupita kiasi, na pia kutakusaidia ukubali matatizo ya maisha bila kuvunjika moyo sana.

Unaweza kupambana na pepo kali za maisha, na ukuwe hakika kama hali itakuwa muzuri tu

 Mambo yenye unaweza kufanya

  •   Ukuwe na mawazo yenye kufaa juu ya makosa yako.

     Biblia inasema kama: “Hakuna mwenye haki katika dunia mwenye anafanya mema sikuzote na hafanyake zambi.” (Muhubiri 7:20) Wakati unafanya makosa ile inaonyesha tu kama uko mwanadamu, haionyeshe kama uko wa bure.

     Namna ya kuwa na mawazo yenye kufaa: Ujikaze kubadilika, lakini usitazamie kama utakuwa mukamilifu. Kijana mwenye kuitwa Caleb anasema hivi: “Ninajikaza kuepuka kufikiri sana juu ya makosa yangu. Kuliko kufanya vile, ninajikaza kujifunza kutokana na makosa yangu ili nifanye mabadiliko.”

  •   Epuka kujilinganisha na wengine.

     Biblia inasema hivi: “Tusikuwe tunajisifu, tusichochee mashindano kati yetu, tusisikiliane wivu.” (Wagalatia 5:26) Wakati unaangalia picha za matukio yote yenye haukualikwa, zenye watu wanatia ku site za Enternete za kupashana habari, unaweza kukasirika na kuvunjika moyo. Ile inaweza kufanya uone marafiki wako wa sana kuwa maadui wako wa sana.

     Namna ya kuwa na mawazo yenye kufaa: Jua kama hawatakualika ku kila karamu. Zaidi ya ile, picha zenye watu wanatia ku site za Enternete za kupashana habari hazionyeshe mambo yote. Kijana mumoja mwenye kuitwa Alexis anasema hivi: “Mara mingi, ku site za Enternete za kupashana habari, watu wanatia picha za matukio ya maana sana ya maisha yao. Mara mingi hawatie picha zenye kuonyesha mambo ya kawaida.”

  •   Ukuwe mutu mwenye kufanya amani, zaidi sana katika familia yako.

     Biblia inasema hivi: “Kama inawezekana, kwa kadiri inawategemea ninyi, mukuwe wenye kufanya amani.” (Waroma 12:18) Hauwezi kuzuia kabisa matendo ya wengine, lakini unaweza kuzuia matendo yako. Unaweza kuchagua kuwa mutu mwenye kufanya amani.

     Namna ya kuwa na mawazo yenye kufaa: Ujikaze sana usiongezee familia yako matatizo, lakini ukuwe mutu mwenye kufanya amani, kama vile ungefanya na marafiki wako. Kijana mumoja mwenye kuitwa Melinda anasema hivi: “Hakuna mutu mwenye iko mukamilifu, na sisi wote tunaweza kukosea wengine kila mara. Ni daraka letu kuamua ikiwa tutafanya amani na wengine ao hapana.”

  •   Ukuwe mwenye shukrani.

     Biblia inasema: “Mujionyeshe kuwa wenye shukrani.” (Wakolosai 3:15) Kuwa mwenye shukrani kutakusaidia ukazie akili mambo ya muzuri katika maisha yako, kuliko kukazia akili mambo yenye haikufurahishe.

     Namna ya kuwa na mawazo yenye kufaa: Kubali kama uko na matatizo, lakini usisahau kama kuko pia mambo ya muzuri katika maisha yako. Kijana mwanamuke mwenye kuitwa Rebecca anasema hivi: “Kila siku, ninaandika jambo moja la muzuri katika buku langu. Ninapenda kujikumbusha kama, hata kama niko na magumu, niko pia na mambo mingi ya muzuri ya kufikiria.”

  •   Chunguza marafiki wako.

     Biblia inasema hivi: “Mashirika ya mubaya yanaharibu tabia za muzuri.” (1 Wakorinto 15:33) Kama unazoea kupitisha wakati pamoja na watu wenye kuwa na tabia ya kuchekelea wengine, ao watu wenye kuweka kinyongo, wewe pia utakuwa na tabia hizo.

     Namna ya kuwa na mawazo yenye kufaa: Wakati marafiki wako wanapata magumu, wanaweza kuhuzunika na kushuka moyo kwa wakati fulani. Uwategemeze, lakini usiache magumu yao ikuhangaishe sana. Kijana mwanamuke mwenye kuitwa Michelle anasema hivi: “Hatupaswe tu kupitisha wakati na watu wenye kuwa na mawazo ya mubaya.”

 Soma habari yenye itakusaidia ukuwe na mutazamo muzuri

 Tunaishi wakati wenye Biblia inaita “nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia.” (2 Timoteo 3:1) Unaona ni nguvu kuwa na mutazamo muzuri katika dunia yenye kujaa magumu? Soma habari yenye kichwa “Juu ya Nini Kuko Mateso Mingi Sana?