Matendo ya Mitume 11:1-30

  • Petro anatoa ripoti kwa mitume (1-18)

  • Barnaba na Sauli katika Antiokia ya Siria (19-26)

    • Wanafunzi wanaitwa Wakristo kwa mara ya kwanza (26)

  • Agabo anatabiri juu ya njaa (27-30)

11  Sasa mitume na ndugu wenye walikuwa Yudea wakasikia kama watu wa mataifa pia walikuwa wamekubali neno la Mungu.  Basi wakati Petro alipanda mupaka Yerusalemu, wale wenye waliunga mukono kutahiriwa+ wakaanza kubishana naye,  kwa kusema: “Uliingia katika nyumba ya watu wenye hawatahiriwe na ukakula pamoja nao.”  Halafu Petro akawaelezea mambo kwa urefu, na kusema:  “Nilikuwa katika muji wa Yopa nikisali, na nikaona katika maono kitu fulani* kinashuka kama kitambaa kikubwa cha kitani, kilikuwa kinateremushwa kutoka mbinguni kwenye pembe zake ine (4), na kikakuja moja kwa moja mupaka mahali nilikuwa.+  Wakati niliangalia ndani yake kwa uangalifu, nikaona wanyama wa dunia wenye miguu ine (4), wanyama wa pori, viumbe vyenye kutambaa, na ndege wa mbinguni.  Nikasikia pia sauti ikiniambia, ‘Petro, simama, chinja na ukule!’  Lakini nikasema, ‘Hapana Bwana, kwa sababu kitu chochote kichafu ao chenye hakiko safi hakijaingia katika kinywa changu hata siku moja.’  Mara ya pili, ile sauti kutoka mbinguni ikajibu: ‘Wewe acha kuita vitu vyenye Mungu ametakasa kuwa ni vichafu.’ 10  Hilo likatokea mara ya tatu (3), na vyote vikakokotwa tena juu kuelekea mbinguni. 11  Wakati uleule pia, wanaume watatu (3) walikuwa wamesimama karibu na nyumba yenye tulikuwa tunakaa ndani; walikuwa wametumwa kwangu kutoka Kaisaria.+ 12  Kisha roho ikaniambia niende pamoja nao, bila kuwa na mashaka hata kidogo. Lakini hawa ndugu sita (6) pia walienda pamoja na mimi, na tukaingia katika nyumba ya mwanaume huyo. 13  “Alituelezea namna alimuona malaika amesimama katika nyumba yake na kusema, ‘Tuma watu waende Yopa waite Simoni mwenye kuitwa Petro,+ 14  na atakuambia namna wewe na watu wote wa nyumba yako munaweza kuokolewa.’ 15  Lakini wakati nilianza kusema, roho takatifu ikawaangukia kama vile ilituangukia pale mwanzo.+ 16  Halafu nikakumbuka maneno ya Bwana, namna alikuwa anasema: ‘Yohana alibatiza kwa maji,+ lakini ninyi mutabatizwa kwa roho takatifu.’+ 17  Kwa hiyo, kama Mungu alipatia hao zawadi ileile ya bure kama vile alitupatia sisi wenye tumemuamini Bwana Yesu Kristo, mimi ni nani ili niweze hata kumuzuia Mungu?”+ 18  Wakati walisikia mambo hayo, wakaacha kupinga,* na wakamutukuza Mungu, na kusema: “Kwa hiyo basi, Mungu amepatia watu wa mataifa pia musamaha wenye unaongoza kwenye uzima.”+ 19  Sasa wale wenye walikuwa wametawanywa+ kwa sababu ya taabu yenye ilitokea juu ya mambo yenye yalimupata Stefano wakaenda mupaka Foinike, Kipro, na Antiokia, lakini walisema lile neno kwa Wayahudi tu.+ 20  Hata hivyo, wamoja kati ya wanaume hao wenye walikuwa wametoka Kipro na Kirene walikuja Antiokia na wakaanza kuzungumuza na watu wenye kusema Kigiriki, wakitangaza habari njema ya Bwana Yesu. 21  Zaidi ya hayo, mukono wa Yehova* ulikuwa pamoja nao, na wengi wakakuwa waamini na wakageuka na kuwa upande wa Bwana.+ 22  Habari juu yao ikafika katika masikio ya kutaniko kule Yerusalemu, na wakamutuma Barnaba+ mupaka Antiokia. 23  Wakati alifika na kuona fazili zenye hazistahiliwe za Mungu, akafurahi na akaanza kuwatia wote moyo waendelee kuwa waaminifu kwa Bwana kwa moyo wote;+ 24  kwa maana Barnaba alikuwa mutu muzuri mwenye kujaa roho takatifu na imani. Na watu wengi sana wakaongezwa kwa Bwana.+ 25  Basi akaenda Tarso ili kumutafuta Sauli.+ 26  Kisha kumupata, akamuleta Antiokia. Basi kwa mwaka muzima wakakusanyika pamoja nao katika kutaniko na kufundisha watu wengi, na ni kule Antiokia ndiko kwa mara ya kwanza wanafunzi waliitwa Wakristo kupitia muongozo wa Mungu.+ 27  Katika siku hizo manabii+ walishuka kutoka Yerusalemu na kuja Antiokia. 28  Mumoja wao mwenye kuitwa Agabo+ akasimama na kutabiri kupitia roho kwamba njaa kali ilikuwa karibu kuja juu ya dunia yote yenye kuikaliwa na watu,+ yenye kwa kweli, ilitokea wakati wa Klaudio. 29  Basi wanafunzi wakaamua, kila mumoja kulingana na uwezo wake,+ kutuma misaada*+ kwa ndugu wenye kuishi Yudea; 30  na walifanya vile, wakatuma misaada kwa wazee kupitia mukono wa Barnaba na Sauli.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “aina fulani ya chombo.”
Tnn., “wakabakia kimya.”
Ao “utumishi wa kupeleka misaada.”