Matendo ya Mitume 20:1-38

  • 20Paulo katika Makedonia na Ugiriki (1-6)

  • Eutiko anafufuliwa kule Troa (7-12)

  • Kutoka Troa kuenda Mileto (13-16)

  • Paulo anakutana na wazee wa Efeso (17-38)

    • Kufundisha nyumba kwa nyumba (20)

    • “Furaha zaidi katika kutoa” (35)

20  Wakati fujo ilitulia, Paulo akatuma watu waite wanafunzi, na kisha kuwatia moyo na kuwaaga, akaanza safari yake ya kuenda Makedonia.  Kisha kupita katika maeneo hayo na kuambia wale wenye walikuwa kule maneno mengi ya kutia moyo, akafika Ugiriki.  Akakaa kule miezi tatu (3), lakini kwa sababu Wayahudi walikuwa wamefanya mupango mubaya juu yake+ wakati alikuwa karibu kusafiri kuenda Siria, akaamua kurudia kwa kupitia Makedonia.  Alienda pamoja na Sopatro mwana wa Piro wa Beroya, Aristarko+ na Sekundo wa Watesalonike, Gayo wa Derbe, Timoteo,+ na kutoka jimbo la Asia, Tikiko+ na Trofimo.+  Wanaume hao wakatangulia na walikuwa wanatungojea kule Troa;  lakini sisi tukaanza kusafiri katika bahari kutoka Filipi kisha Sikukuu ya Mikate Yenye Haina Chachu,+ na kwa siku tano (5) tukawakuta kule Troa, na tukakaa kule siku saba (7).  Siku ya kwanza ya juma, wakati tulikuwa tumekusanyika pamoja ili kula chakula, Paulo akaanza kuwatolea hotuba, kwa sababu alipaswa kuondoka siku yenye ilifuata; na akarefusha hotuba yake mupaka katikati ya usiku.  Basi kulikuwa taa nyingi katika chumba cha juu kwenye tulikuwa tumekusanyika.  Kijana mumoja mwanaume mwenye kuitwa Eutiko alikuwa amekaa kwenye dirisha, na alikuwa amelala usingizi muzito wakati Paulo alikuwa anazungumuza, na kwa sababu ya usingizi, akaanguka chini kutoka kwenye gorofa ya tatu (3) na akaokotwa akiwa amekufa. 10  Lakini Paulo akashuka kutoka kwenye gorofa, akajitupa juu yake na akamukumbatia,+ na kusema: “Muache kuhuzunika, kwa maana yeye ni muzima.”*+ 11  Akapanda kwenye gorofa na akaanzisha chakula* na akakula. Akaendelea kuzungumuza kwa wakati murefu, mupaka asubui sana, na kisha akaondoka. 12  Basi wakamubeba ule kijana mwanaume akiwa muzima, na wakafarijika sana. 13  Sasa tukaenda kwenye mashua* na tukasafiri katika bahari mupaka Aso, kwenye tulikusudia kumubeba Paulo katika mashua, kwa maana kisha kutuagiza vile, alikusudia kuenda kule kwa miguu. 14  Basi wakati alitukuta kule Aso, akapanda katika mashua* pamoja na sisi na tukaenda Mitilene. 15  Kesho yake tukasafiri katika mashua* kutoka kule, tukafika sehemu za Kio, lakini siku yenye ilifuata tukasimama Samo kwa wakati kidogo, na siku yenye ilifuata, tukafika Mileto. 16  Paulo alikuwa ameamua kuendelea na safari bila kupitia Efeso,+ ili asipitishe wakati wowote katika jimbo la Asia, kwa maana alikuwa anafanya haraka ili afike Yerusalemu+ siku ya Sikukuu ya Pentekoste kama ingewezekana. 17  Lakini, akiwa Mileto, akatuma watu waende Efeso waite wazee wa kutaniko. 18  Wakati walifika kwenye alikuwa, akawaambia: “Munajua muzuri namna nilijiendesha mwenyewe kati yenu tangu siku ya kwanza yenye nilikanyanga katika jimbo la Asia,+ 19  namna nilimutumikia Bwana kwa unyenyekevu wote*+ na machozi na majaribu yenye yalinipata wakati Wayahudi walifanya mupango mubaya juu yangu, 20  na sikuepuka kuwaambia ninyi jambo lolote lenye faida na kuwafundisha mbele ya watu wote+ na nyumba kwa nyumba.+ 21  Lakini nilitoa ushahidi kikamili kwa Wayahudi na Wagiriki pia juu ya kutubu+ kwa Mungu na kumuamini Bwana wetu Yesu.+ 22  Na sasa, muangalie! nikiwa nimefungwa katika* roho, ninasafiri kuenda Yerusalemu, hata kama sijue ni mambo gani yatanipata kule, 23  isipokuwa kwamba kutoka muji mupaka muji roho takatifu inanitolea ushahidi tena na tena, ikisema kama gereza na taabu vinaningojea.+ 24  Hata hivyo, sione uzima wangu mwenyewe kuwa wa* maana sana kwangu,* jambo la maana kwangu ni kumaliza mwendo wangu+ na utumishi wenye nilipokea kutoka kwa Bwana Yesu, kutoa ushahidi kamili juu ya habari njema ya fazili zenye hazistahiliwe za Mungu. 25  “Na sasa, muangalie! Nilihubiri kati yenu juu ya Ufalme, lakini kuanzia sasa na kuendelea hakuna hata mumoja wenu mwenye ataona tena uso wangu. 26  Basi nimewaita ili mushuhudie leo hii kwamba niko safi kutokana na damu ya watu wote,+ 27  kwa maana sikuepuka kuwaambia ninyi shauri lote* la Mungu.+ 28  Mujiangalie ninyi wenyewe+ na kundi lote, lenye roho takatifu imewaweka ninyi kuwa waangalizi kati yake,+ ili kuchunga kutaniko la Mungu,+ lenye alinunua kwa damu ya Mwana wake mwenyewe.+ 29  Ninajua kwamba kisha mimi kuondoka imbwa wa pori wenye kukandamiza wataingia katikati yenu+ na hawatatendea kundi kwa upole wote,* 30  na kutoka katikati yenu wenyewe, watu watasimama na kusema mambo yenye kupotoka ili kuvuta wanafunzi wawafuate.+ 31  “Kwa hiyo muendelee kukesha, na mukumbuke kwamba kwa miaka tatu (3),+ usiku na muchana, sikuacha kumuonya kila mumoja wenu kwa machozi. 32  Na sasa ninawatia katika mikono ya Mungu na ya neno la fazili zake zenye hazistahiliwe, neno lenye linaweza kuwajenga na kuwapatia uriti kati ya wale wote wenye walitakaswa.+ 33  Sikutamani feza, zahabu, ao nguo ya mutu yeyote.+ 34  Ninyi wenyewe munajua kwamba mikono hii imenisaidia mimi+ na wale wenye kuwa pamoja na mimi kupata mambo yenye tuko nayo lazima. 35  Nimewaonyesha ninyi katika mambo yote kwamba kwa kufanya kazi kwa bidii kwa njia hiyo,+ munapaswa kusaidia wale wenye kuwa wazaifu, na munapaswa kuweka katika akili maneno ya Bwana Yesu, wakati yeye mwenyewe alisema: ‘Kuko furaha zaidi katika kutoa+ kuliko katika kupokea.’” 36  Na wakati alimaliza kusema mambo hayo, akapiga magoti pamoja nao wote na kusali. 37  Kwa kweli, wote wakalia sana, na wakamukumbatia Paulo* na kumubusu kwa upendo mwingi,* 38  kwa maana waliumizwa sana na neno lenye alikuwa amesema, kwamba hawataona tena uso wake.+ Kisha wakamusindikiza mupaka kwenye mashua.*

Maelezo ya Chini

Ao “nafsi yake iko ndani yake.”
Tnn., “akavunja mukate.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “unyenyekevu wote wa akili.”
Ao “nimechochewa na.”
Ao “nafsi yangu mwenyewe kuwa ya.”
Ao “kuwa wenye samani yoyote kwangu.”
Ao “kusudi lote.”
Ao “wororo.”
Tnn., “wakamuangukia Paulo kwenye shingo.”
Ao “kwa wororo; kwa upole wote.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”